Habari za hivi Punde

WATU 31 WAFARIKI KUTOKANA NA UGONJWA WA EBOLA.

 

Watu 30 wamefariki kutokana na Ebola DRC
Shirika la afya duniani likishirikiana na wizara ya afya katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imesema kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini humo umewaua watu 31.
Ugonjwa huo ulipatikana mapema mwezi uliopita katika nchi hiyo karibu na mji wa Boende takriban kilomita mia nane kazkazini mwa mji mkuu wa Kinshasa.

Maafisa wanasema kuwa eneo hilo limewekwa karantini na zaidi ya watu 50 wanapokea matibabu baada ya kuambukizwa maradhi hayo.

Takriban watu 200 wanachunguzwa. Wizara ya afya mjini Kinshasa imesisitiza kuwa mlipuko wa homa hiyo haihusishwa na mlipuko wa Ebola uliotikisa kanda ya Afrika Magharibi ambako zaidi ya watu 1500 wamefariki.

0 Response to "WATU 31 WAFARIKI KUTOKANA NA UGONJWA WA EBOLA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.