Habari za hivi Punde

DREVA WA BODABODA AUAWA KIKATILI KISHA MWILI WAKE KUTELEKEZWA KANISANI.

Kijana mwendesha pikipiki akibeba abiria maarufu kama (Boda boda) katika manispaa ya Tabora ameuawa na watu wasiojulikana na kumtelekeza aneo la kanisa katholiki Makokola, na kutoweka na pikipiki yake aina ya Sanlg huku kisu kilichodaiwa kutumika kumuua kikitelekezwa eneo hilo.
Akizungumza kwa masikitiko eneo la tukio alipouawa mwendesha pikipiki huyo, katibu wa chama cha waendesha Bodaboda Bw.Kasim Kiduli amesema kuwa, matuikio ya kukatisha maisha ya waendesha pikipiki inaonesha kurudi mkoani Tabora, kwani kulikuwa na ukimya kwa muda.
Baadhi ya wananchi wakiokuwa katika tukio hilo pamoja na kukemea tabia ya mauaji, wamewataka waendesha pikipiki hao kujihadhari na kutofanya kazi nyakati za usiku, kwani katika kubeba unaweza kumbeba adui bila kumjua.
Kamanda wa polisi mkoani Tabora kamishina  msaidizi Suzani Kaganda, amemtaja marehemu kwa jina la Cosmas John, amesema kuwa, pamoja na kifo hicho, katika hali isiyokuwa ya kawaida watu wasiojulikana wamewaua mama na watoto wake wawili  wanafunzi wa shule ya msingi Mwamalulu wilayani Nzega.

0 Response to "DREVA WA BODABODA AUAWA KIKATILI KISHA MWILI WAKE KUTELEKEZWA KANISANI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.