Habari za hivi Punde

RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AFARIKI DUNIA



HATIMAYE baada ya kuibuka uvumi siku ya Jumanne kuamkia Jumatano juu ya kufariki kwa rais wa Zambia Michael Sata, Serikali ya nchi hiyo imethibitisha kifo chake.

Kwa mujibu wa katibu wa baraza la mawaziri, Roland Msiska amethibitisha kifo hicho  cha Sata {77}  kilichotokea baada ya rasi huyo kusafirii kuelekea jijini London Uingereza juma moja lililopita kwaajii ya kupata matibabu.
Akitoa tangazo hilo alfajiri, Roland aliwaambia wananchi wa Zambia kwa masikitiko makubwa angependa kutangaza kifo cha rais wao aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Uingereza.
Tangazo hili linathibitisha madai ya vyama vya upinzani na watu wa karibu wa rais Sata ambao mara kadhaa walidai kuwa kiongozi huyo anaugua na ameshindwa kutekeleza majukumu yake kama rais lakini mara zote Serikali imekuwa ikikanusha hadi juma moja lililopita ilipothibitisha kuugua kwa rais Sata.
Wakati alipokuwa akiondoka kuelekea jijini London kwa matibabu, rais Sata alimteua waziri wa ulinzi na sheria Edgar Lungu kukaimu madaraka ya rais kwa kipindi ambacho hatokuwepo.
Makamu wa rais Guy Scott ambaye mara kadhaa amekuwa akishiriki shughuli mbalimbali za Serikali kama kiongozi wa nchi, yeye ana uraia wa Uskochi hali ambayo inamfanya ashindwe kuwa rais kamili wa taifa la Zambia kwakuwa wazazi wake hawakuzaliwa nchini Zambia.
Sata ambaye alibatizwa jina la "King Cobra" na wafuasi wake wakati alipochaguliwa mwaka 2011, alionekana kama mbadala wa siasa za Zambia na mtu ambaye alikuwa wavitendo licha ya kukosolewa kwa sehemu kubwa na upinzania.
Hivi karibuni rais Sata alianza operesheni dhidi ya wapinzani wake na waandishi wa habari wlaiokuwa wakikosoa Serikali yake jambo ambalo lilianza kumchora kama mmoja wa viongozi wababe kusini mwa bara la Afrika.

0 Response to "RAIS WA ZAMBIA MICHAEL SATA AFARIKI DUNIA "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.