Habari za hivi Punde

UMILIKI WA ARDHI CHANZO CHA KUTONUFAISHA WAJASILIAMALI.

UMILIKI WA ARDHI CHANZO CHA KUTONUFAISHA WAJASIRIAMALI

MENEJA wa Azania Tawi la Kahama,Godfrey Mahona akiongea.


IMEDAIWA kuwa tatizo la umiliki wa ardhi katika maeneo yasiyo pimwa na mpango miji yakiwemo ya vijijini ni sababu inayokwamisha wajasiliamali wengi kukosa fursa ya kupata mikopo
mikubwa kutoka kwenye vyombo vya fedha


Hayo yalibainishwa na Meneja wa benki ya Azania tawi la Kahama Godfrey Mahona wakati akitoa maada ya mafunzo ya ujasiliamali kwa wafanyabiashara wa kata ya Bulyanhulu wilayani Kahama yaliyofanyika kwenye kijiji cha Kakola Halmashauri ya Msalala


Meneaja huyo alisema tatizo hilo la kutopimwa kwa maeneo ya ardhi ya vijijini imechangia kwa kiwango kikubwa kuwakosesha umiliki wa kudumu na hivyo kuwa chanzo cha baadhi ya wajasiliamali kuambulia wasitani wa mkopo wa Shilingi Milioni kumi badala ya kupata fedha zaidi ya Milioni 50


Awali mwenyekiti wa wajasilamali hao Robert Zungu aliwaomba  wafanyabiashara wenzake kutumia fursa ya mafunzo hayo yanayotolewa na Benki ya Azania ambayo yatawasaidia kupata elimu ya kuweza kukopa na kurejesha kwa muda kuwa chachu ya kukomboka kimtaji na kupiga hatua za kiuchumi kupitia miradi yao.


Kufuatia hali hiyo Mahona alisema upo umuhimu  wa Benki yake kuwasaidia wajasiliamali hao kupimiwa maeneo yao ambapo halmashauri ya wilaya husika inaweza kuingia mkataba na taasisi yake juu ya ulejeshwaji wa gharama za kupimiwa  ambapo kila mwananchi mwenye mahitaji hayo anaweza kuchangia

0 Response to "UMILIKI WA ARDHI CHANZO CHA KUTONUFAISHA WAJASILIAMALI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.