Habari za hivi Punde

VITUKO VIMETAWALA MWENGE WA UHURU MKOANI SHINYANGA ANGALIA PICHA ZAIDI

 Hapa ni katika kijiji cha Mwabomba (mnadani) kata ya Idahina halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambako leo mwenge wa uhuru umepokelewa na katibu tawala mkoa wa Shinyanga Dkt Anselm Tarimo ukitoka Geita.Katibu tawala mkoa wa Geita Severine Kahitwa amekabidhi kwa katibu tawala mkoa wa Shinyanga ambaye naye kakabidhi kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya .Mwenge huo leo upo Ushetu,kesho mji Kahama kesho kutwa Msalala. Ukiwa Shinyanga jumla ya miradi 58 yenye thamani ya shilingi bilioni 7.6 itazinduliwa-Picha zote na Kadama Malunde

Huyu ni mtu_ Moja ya kati ya burudani zilizokuwepo wakati wa mapokezi ya mbio za mwenge wilayani Kahama leo,ambapo mwenge huo utakimbizwa katika halmashauri 6 za mkoa wa Shinyanga yaani Ushetu,Kahama mji,Msalala,Shinyanga,manispaa ya Shinyanga na Kishapu sawa na kilomita  1188
Mcheza ngoma ya Mashanga kutoka kijiji cha Nundu kata ya Chela halmashauri ya Ushetu akifanya yake
Ngoma ya Wagoyangi,jamaa anacheza na nyoka
Eneo la mapokezi ya Mwenge wa uhuru leo Shinyanga
Viongozi mbalimbali wa mkoa w Shinyanga wakijiandaa kupokea mwenge wa uhuru leo
Wanafunzi walijitokeza kwa wingi
Tunasubiri Mwenge......
Burudani inaendelea,akina mama kutoka Kahama wakifanya yao
Wanafunzi wa shule ya msingi Mwabomba wakicheza viduku

Mama huyu mjamzito uvumilivu ulishinda akajitokeza kucheza wimbo wa Bhudagala" Kundi Wa Ng'wamoto"

Shamra shamra za mwenge wakazi wa Mwabomba walijitokeza kwa wingi,wengine wakapanda juu ya miti
Kutoka Geita-Mwenge Unaletwa Shinyanga
Mwenge unawasili Mwabomba
 Mwenge uko Mwabomba
 Mwenge ukiwa eneo la mapokezi Mwabomba Kahama
Shamra shamra za mwenge zinaendelea
Katibu tawala mkoa wa Geita Severine Kahitwa akisoma taarifa kabla ya kukabidhi mwenge mkoa wa Shinyanga



0 Response to "VITUKO VIMETAWALA MWENGE WA UHURU MKOANI SHINYANGA ANGALIA PICHA ZAIDI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.