Habari za hivi Punde

WANANCHI WATAKIWA KUWAPA MAENDELEO YA ELIMU WATOTO WAO

KADA WA CCM WILAYANI MASWA MKOANI SIMIYU   STANSLAUS  NYONGO.

WANANCHI na wadau mbalimbali katika wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu wametakiwa kujitolea katika masuala ya elimu na maendeleo na kuacha kuchangia mambo mengine yasiyokuwa na tija.
Hayo yalielezwa jana na Kada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)wilaya ya Maswa ,Stanslaus Nyongo katika mahafali ya kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Shishiyu iliyoko wilayani humo.

Alisema wazazi wanatakiwa kuhakikisha wanawarithisha watoto wao elimu na si kitu kingine kwani kufanya hivyo kunawaandalia maisha yaliyo bora.
“Mafanikio ya wanafunzi wetu ni mafanikio kwa taifa hivyo tunatakiwa kuhakikisha wanapata elimu iliyo bora kwa kushirikiana kwa pamoja,” alisema
Nyongo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo alisema kuwa wazazi hao  wana wajibu na ulazima wa kuhakikisha kwamba watoto waowanawasimamia vyema katika kupata elimu bora itakayotoa mwanga wa kimaisha katika hatma yao ya baadaye. 
Alisema jukumu la kuhakikisha mtoto anapata elimu si la serikali pekee bali ni wazazi na wadau mbalimbali kuungana kwa pamoja.
“Urithi pekee ambao mzazi au taifa linatakiwa kuutoa kwa watoto ni elimu nanyi watoto mnatakiwa kuacha anasa na kuweka akili zenu katika masomo,acheni kucheza michezo isiyokuwa na tija kama ‘game’ na matumizi ya simu ambayo yanawaathiri kwa sehemu kubwa ili mtakapofika wakati wa kufanya mitihani mfanye vizuri”.Alisema.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa shule hiyo, Godlisten Kabarata alisema kuwa tangu kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2006 ya Kata ufaulu umekuwa ukiongezeka kwa wanafunzi wa kidato cha nne na kwa mwaka uliopita shule hiyo ilishika nafasi ya kwanza ya katika wilaya hiyo kati ya shule 38.
Katika Mahafali hayo jumla ya Shilingi 1,700,000/=zilikusanywa kwa ajili ya kuweka umeme katika vyumba vya madarasa na nyumba za walimu ambapo mgeni Rasmi alichangia  fedha taslimu kiasi cha shilingi 500,000/= na wanafunzi 83 wakiwemo wavulana 53 na wasichana 30 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu.

0 Response to "WANANCHI WATAKIWA KUWAPA MAENDELEO YA ELIMU WATOTO WAO"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.