Habari za hivi Punde

WAZEE MKOANI SHINYANGA WAOMBA MIKOPO YENYE MASHART NAFUU




WAZEE mkoani Shinyanga  wameiomba serikali kuwapatia mikopo  yenye mashart nafuu ili waweze kujinyanyua kiuchumi  kutokana na kuishi maisha yenye umasikini uliokithiri nakuwa tegemezi katika familia.

Wazee hao  waliyasema hayo  katika kikao cha kuhamasisha vyombo vya habari kuhusu masuala ya wazee  kwa waandishi wa habari kilichoandaliwa na taasisi  isiyo ya kiserikali inayoongozwa na wanawake wenye taaluma ya kilimo na mazingira  (Tawlae)  inayojishughulisha na masuala ya wazee.


Wazee hao kupitia kamati ya  baraza la wazee waliomba serikali  kupatiwa mikopo yenye mashart nafuu kwa wazee ili waweze kujikimu kimaisha.

Mmoja wa wazee hao  John Kikulwa kutoka kijiji cha Ibingo kata ya Samuye  alisema kuwa wazee bado hawajapewa kipaumbele katika jamii asilimia kubwa wamekuwa walezi wa familia huku wakiishi maisha duni  nakukosa mikopo.

Mwenyekiti wa baraza la wazee   halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Edward  Lupimo  alisema kuwa wazee  wanaishi maisha ya kimasikini ambapo kwa hivi sasa  baadhi yao wamepata unafuu kwa kupitia mlango wa mfuko wa hifadhi ya jamii (Tasaf)  kupata msaada na kujiongezea kipato.

Afisa maendeleo ya jamii  wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga   Joram  Magana alitoa ushauri kwa wazee  kuwa wanatakiwa kuunda vikundi vitakavyo tambulika  kwenye halmashauri ili waweze kupatiwa mikopo.

“Lengo la serikali ni kila mmoja kuishi maisha bora nanyi mtakapo unda vikundi inatakiwa vitambulike ndipo muombe mikopo kwa kuanzisha miradi ya kikundi  kama ufugaji au kilimo hapo hapo  mkiiomba wataalamu waje kwenye vikundi hivyo wawapatie elimu”alisema .

Naye katibu wa taasisi ya Tawlae  Hellen Maleza alisema kuwa  wanaishukuru tasaf   kwa kutoka msaada huo kwani hata baadhi ya wazee walinufaika, pia  wametakiwa  kupokea ushauri wa kuanzisha vikundi nakuvisajiri ili waweze kutambulika kwenye halmashauri.

0 Response to "WAZEE MKOANI SHINYANGA WAOMBA MIKOPO YENYE MASHART NAFUU"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.