Habari za hivi Punde

WAHITIMU CHUO KIKUU HURIA WAMEELEZWA KUITUMIA ELIMU HIYO KWA MANUFAA YA UMMA


WAHITIMU wa chuo  kikuu huria tawi la Shinyanga ambao baadhi  ni  watumishi wa umma wametakiwa kuitumia elimu walioipata kwa kuondoa changamoto zilizopo kwenye jamii na kunyanyua uchumi.
Hayo yalisemwa jana  na  afisa elimu  msingi manispaa ya Shinyanga  Paul Magubiki  aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafari ya tano  kwa tawi hilo lililojumuisha wahitimu 126 kwa ngazi mbalimbali.

Magubiki alisema kuwa  anatambua kuwa baadhi ya wahitimu katika kozi mbalimbali ni wafanyakazi wa serikali  kwenye utumishi wa umma  hivyo waitumie elimu hiyo  kuisaidia jamii kuongeza uchumi ikiwemo kutatua changamoto zinazo ihusu jamii.
“Taifa hili litaweza kuinua uchumi wake kulingana na watu wake wanavyofanya kazi  changamoto zilizopo  zijaribu kupunguzwa kwa kutumia elimu waliyonayo kwa utumishi uliotukuka,  kwani  watumishi hao ndio watekelezaji wa maisha ya kila siku  kwenye jamii hilo linawezekana”alisema Magubiki.
Alisema elimu kupitia masafa  ya mbali yameweza  kutoa elimu kwa watumishi  kwa kuwafanya waendelee na kazi  huku wakipata elimu,hata wasio watumishi  waliombali na maeneo  ya chuo  waliweza kunufaika na masomo  yanayotolewa hivyo hakuna budi kuitangaza elimu kwa njia ya masafa.
Naye mkurugenzi wa tawi hilo  Martha  Kabate  alisema kuwa  chuo hicho kwa mkoa wa Shinyanga kilianza rasmi mwaka 2006  kikiwa na jumla ya wanafunzi 11 hadi kufikia mwaka 2015 wahitimu wamefikia 126  hali inaonyesha mwamko wa kupata elimu ya juu kwa njia hiyo umeanza kufanikiwa.
“Ukiangalia  mwamko wa elimu  ya juu  kwa njia ya masafa  ya mbali  umeanza kuonekana  katika jamii kwani mwaka 2006 waliohitimu ni wanafunzi 11 huku mwanamke akiwa mmoja ambapo mwaka 2015 wamehitimu wanafunzi  126 huku  wanaume wakiwa 72 na wanawake 54 ila bado kunachangamoto ya uhaba wa viti na meza za kujisomea chuoni hapo”.alisema Kabate. 
Kwa upande wake  mwenyekiti wa chuo hicho  Eustadius  Mkulu akisoma risala kwa niaba ya wanachuo alisema kuwa  mafanikio waliyoyapata ni mengi kwa kuweza pia kumudu kwa kujisomea  bila walimu kwa kupitia njia za mitandao
Naye Magayane Desidery ni mfanyakazi wa jeshi la wananchi aliyehitimu digirii ya kwanza ya sheria  alisema kuwa  alishawishika kujiendeleza ili kuweza kutatua changamoto mbalimbali za kijamii huku akiwashauri wafanyakazi wenzake kuweza kujiendeleza.


0 Response to "WAHITIMU CHUO KIKUU HURIA WAMEELEZWA KUITUMIA ELIMU HIYO KWA MANUFAA YA UMMA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.