Habari za hivi Punde

ASILIMIA 70 YA WAFANYAKAZI MGODINI HUFUKUZWA KAZI KINYUME CHA SHERIA YA SEKTA YA MADINI NCHINI.



Na  Kareny   Masasy
Shinyanga.

MELEZWA kuwa asilimia   70  ya wafanyakazi wa Migodi hufukuzwa kazi  kinyume cha  sheria na wawekezaji wa nje ya nchi wanaowekeza katika sekta ya Madini 

Hayo yameelezwa na Hassan  Amir  katibu mkuu taifa  wa Chama cha wafanyakazi wa Migodi,  Nishati na Ujenzi (TAMICO)  alipokuwa akihuhutubia mkutano mkuu maalumu kanda ya Shinyanga uliofanyika mjini hapa.

Amir amesema  Uongozi wa Migodi ambao unaongoza kuwafukuza wafanyakazi wake ni pamoja na Bulyanhulu na Buzwagi ambapo kwa kipindi cha januari hadi disemba mwaka huu zaidi ya wafanyakazi 80 walifukuzwa kazi kinyume cha sheria za kazi.

Akifafanua amesema  katika mgodi wa Bulyanhulu pekee wafanyakazi 50 walifukuzwa kazi na katika mgodi wa Buzwagi wafanyakazi 35 walifukuzwa kazi baada ya afya zao kuzorota baada ya kuugua kutokana na madawa mbalimbali yenye sumu ambayo hutumika migodini.

Amesema  katika kipindi cha mwaka 2013 kesi 70 zilifunguliwa katika ofsi za idara ya kazi na kesi zingine 15 zimefunguliwa mahakama kuu za hapa nchini huku zikisimamiwa na  tamico na kupata ushidi.

Wakati huohuo  wajumbe wa  mkutano huo ulimchagua Antony Masonda kuwa mwenyekiti wa kanda ya Shinyanga na Clioford Wambura alichaguliwa kuwa  mjumbe wa baraza kuu la Taifa.

Katika nafasi ya Mwenyekiti wa kamati ya vijana wa kanda alichaguliwa   Pius Mashimba wakati   Shija Golani na Vaileth Matanga walichaguliwa kuwa wajumbe wa kamati ya utendaji kanda ya Shinyanga.


0 Response to "ASILIMIA 70 YA WAFANYAKAZI MGODINI HUFUKUZWA KAZI KINYUME CHA SHERIA YA SEKTA YA MADINI NCHINI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.