Habari za hivi Punde

PACESHI YATOA MAFUNZO KWA WASAIDIZI WA KUFIKISHA ELIMU YA KISHERIA KWENYE MAENEO YA PEMBEZONI




 Na  Kareny  Masasy
Shinyanga

SHIRIKA  lisilo la kiserikali PACESHI linalotoa msaada wa kisheria mkoani Shinyanga limetoa mafunzo kwa wasaidizi 25 ambao watasaidia kufikisha elimu ya kisheria katika jamii iliyoko maeneo ya vijijini ili waweze kupata haki zao za msingi zinazoelekea kupotea ama zilizopotea.

Akitoa mafunzo hayo mkurugenzi wa shirika hilo jana Perpetua Magoke alisema mafunzo hayo yatawasaidia kutoa elimu katika jamii zilizoko kijijini zinazogusa maslahi ya kifamilia  kijamii, pamoja na migogoro ya ardhi.

“Watu wengi hasa walioko katika maeneo ya vijijini hawazijui haki zao za kisheria hivyo tumeona kuanzisha mafunzo haya kwa watu 25 kila wilaya ili waweze kufikishiwa elimu ambayo itasaidia wananchi kuondokana na migogoro mbalimbali  inayojitokeza”Alisema Magoke.

Alisema wanawake wamekuwa wakikosa fursa ya kurithi mali wakati mme akifa hivyo waliopata mafunzo hayo watasaidia kutoa elimu na kuweza kuzijua sheria na kuondoa migogoro ya urithi ili kuweza kukuza uchumi wao binafsi.

Kwa upande wake afisa mipango mahusiano na mafunzo John Shija alisema jamii ikipata elimu itasaidia kuondoa ukatili wa kijinsia katika makundi, mbalimbali yakiwemo ya wanawake ,watoto,walemavu, wazee,watu wanaoishi na virusi vya ukimwi pamoja na masikini wa kipato.

Shija alisema makundi hayo yamekuwa yakiathilika sana kulingana na mazingira wanayoishi katika jamii hivyo ambapo shilika la PACESHI linajaribu kuamsha mambo ambayo yatalinda maslahi yao.

“Shirika letu linashughulikia mambo mbalimbali zikiwemo sheria za makosa ya jinai kanuni ya adhabu,sheria zinazohusu mirathi , sheria za ndoa, sheria ya kudhurumiwa sheria za kudhibiti ukimwi, na sheria mbalimbali zitakazosaidia jamii zikifanikiwa makundi haya ya takuwa salama kiulinzi”alisema Shija.

“Pia tunajaribu kuangalia sheria za ardhi zinaoweza kuwalinda wananchi wakizijua sheria hizo ambazo zimekuwa ni tatizo kubwa katika jamii itasaidia kupunguza migogoro iliyokithili ambayo inasababisha watu wengi kukatana na mapanga”aliongeza Shija.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Antony Salamba alilishukru Shirika la PACESHI kwa kuanzisha mafunzo hayo kwani itasaidia kuondoa changamoto za migogoro mbalimbali zinazojitokeza katika maeneo ya vijijini kwani wataenda kutoa elimu na kuweza kutoa ushauri kwa wanakijiji.

 Mafunzo hayo yaliyowahusisha washiriki 25 kutoka katika kata mbalimbali katika wilaya ya Shinyanga yanaendelea kufanyika katika ukumbi wa Diamond Hotel mjini Shinyanga yatafanyika kwa siku 25 .
Mwisho.

0 Response to "PACESHI YATOA MAFUNZO KWA WASAIDIZI WA KUFIKISHA ELIMU YA KISHERIA KWENYE MAENEO YA PEMBEZONI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.