Habari za hivi Punde

DIWANI ALALAMIKA KUPUNJWA KWA FEDHA ZILIZOTOLEWA KWAAJILI YA MRADI WA KUENDELEZA MAJENGO MATATU YA SHULE YA MSINGI IHUGI



Na  Kareny  Masasy
Shinyanga.

 Zaidi ya Shilingi millioni 287 zilitolewa na serikali kuu katika bajeti ya fedha  ya mwaka  2012/13 ikiwa ni mpango wa  kuendeleza miradi ya majengo ya shule za msingi ,nyumba za walimu  katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  ambapo   shule ya msingi  Ihugi  kata ya Lyamidati imelalamikiwa  kupata  fedha  pungufu na kiasi kilichotengwa.

Hayo  yamesemwa jana  na diwani  Leo Mayiku  kutoka kata hiyo  wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Shinyanga huku akieleza kuwa shule hiyo ilipata kiasi cha shilingi  millioni 16.5  kwaajili ya kuendeleza mradi wa madarasa matatu .

Alisema  kuwa licha ya kutengewa fedha hizo kiasi  cha zaidi ya shilingi lakini nne zimeonekana  kutolewa na kushindwa kuelewa zimekwenda wapi huku akidai kuwa pesa hizo ni nyingi zingeweza kuendeleza ujenzi mwingine unaohitajika shuleni hapo. 

“Mimi kama diwani nitahakikisha nafuatilia fedha hizo zilichukuliwa na kwenda wapi ikiwa niliwauliza wahusika waliokwenda kuchukua benki na kuonyesha maelezo  ya risiti  ambao ni mkuu wa shule hiyo Mesoya na  mwenyekiti wa kamati ya  shule  Leonadi Gwangutebe wakidai walichukua  na kukuta  kiasi cha fedha  hicho.”alisema Diwani.

Naye  mwalimu  mkuu wa shule hiyo Ayoub Mesoya alisema kuwa  wao walipokea kiasi ambacho walichokikuta benki  hawakufahamu mapungufu yaliyojitokeza  ila walimuelezwa diwani  kiasi  cha fedha walichokitoa benki  na vielelezo vyote ambapo ilikuwa  imekosekana zaidi ya shilingi laki nne.

Pia alisema kuwa mpaka sasa kuna uhaba wa vyoo vya walimu na matundu ya vyoo vya wanafunzi kwani matundu yaliyopo kwa upande wa wanafunzi ni manne  ambayo hayatoshelezi huku walimu wakikosa choo na kwenda kupata huduma hiyo katika choo cha familia ya mwalimu mkuu.

Kwa upande wake mkurugenzi wa  halmashauri hiyo Kiyungi Mohamedi alisema kuwa  malalamiko hayo ameyasikia kutoka kwa diwani ambapo halmashauri inachukua jukumu la kukagua  fedha zote zilizoingizwa  katika kuendeleza  miradi ya shule za msingi ili kuona mapungufu yaliyojitokeza kama ni sahihi kweli kupata kiasi hicho.

Ambapo Kiyungi  alisema kuwa  jumla ya shule  za msingi  32 zilitengewa kiasi   cha zaidi ya shilingi millioni 287  katika bajeti yake ya kipindi cha mwaka 2012/13  kwa lengo la kukamilisha majengo  ya shule  pamoja na nyumba za walimu yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi.

0 Response to "DIWANI ALALAMIKA KUPUNJWA KWA FEDHA ZILIZOTOLEWA KWAAJILI YA MRADI WA KUENDELEZA MAJENGO MATATU YA SHULE YA MSINGI IHUGI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.