Habari za hivi Punde

BAADHI YA WATUMISHI MANISPAA WADAIWA KUIHUJUMU KWA KUIBA NYARAKA ZA SIRI









BAADHI  ya watumishi katika halmashauri ya manispaa ya Shinyanga wameanza kuihujumu manispaa hiyo kwa kutumia mbinu ya kufungua kesi dhidi ya manispaa hiyo na kuiba nyaraka za ofisi ili kujipatia kipato.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani  naibu mstahiki meya  David Nkulila  alisema  hivi sasa halmashauri hiyo inaandamwa na kesi nyingi za ajabu  zenye lengo la kuihujumu  manispaa kwa  kushindwa kuiba mapato matokeo yake kutumia mbinu hizo.


Alisema manispaa  inataka kuchezewa na watu kwa kuanza kuihujumu kwa kuanzisha makosa yasiyoeleka na kwamba kwa mujibu wa taarifa zinazohisiwa,zinazotia mashaka hujuma hizo zinafanywa na watumishi wa halmashauri hiyo.

“Data zinazohisiwa,zinazosemekana,zinazotia mashaka,watumishi wanahusika,Kesi nyingi sasa zinataka kuiandama halmashauri,mdau yupo anaambiwa anzisha kesi na kesi inaenda kushindikana,mtu huyo anadai alipwe na halmashauri, na hayo madai yanavyosemekana ni mgao wa watu,hizo ni hujuma kwa pesa za wananchi”,alieleza Nkulila.

Akifafanua zaidi alisema menejimenti ya manispaa hiyo imekosa nidhamu ya siri kwani wamekuwa wakitoa nyaraka za siri na kwamba sasa wamebuni njia nyingine ya ulaji kwa kuanzisha kesi badala ya kuwajibika.

Pia   aliwataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa nidhamu,kuridhika na walichonacho,kuwatumikia wananchi na kuwajibika kila mtu kwa nafasi yake kama inavyopaswa kwa kufuata yaliyoelekezwa.

Naye katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniface Chambi aliwataka watumishi wa umma kutunza siri za ofisi na endapo mtu anaona kazi ya serikali ni ngumu aondoke taratibu badala ya kuchezea nyaraka za serikali.

0 Response to "BAADHI YA WATUMISHI MANISPAA WADAIWA KUIHUJUMU KWA KUIBA NYARAKA ZA SIRI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.