Habari za hivi Punde

KIWANDA CHA KUSINDIKA NYAMA CHAANZA MAZUNGUMZO NA WAFUGAJI KWENYE VIKUNDII



HATIMAYE kiwanda cha  kusindika nyama cha Triple  ‘S’ kilichopo manispaa ya Shinyanga kimeanza  kuingia mkataba  kwenye   vikundi vidogo vidogo vya wafugaji  vilivyopo mkoani hapa kwa lengo la kuwanyanyua kiuchumi  huku kikiwa kimekwisha pata soko la uuzaji nyama hizo nchi ya Uarabuni.

Hayo yalisemwa na mmiliki wa  kiwanda hicho Salum Seif mbele ya waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi  Titus Kamani  wakati wa ziara yake mkoani humo na kutembelea kiwanda hicho huku akieleza kuwa  anatarajia kukifungua  na kuanza kazi  mwezi Marchi mwaka huu  ikiwa ataanzia  na ng’ombe 50.

Alisema  wamekuwa na maongezi katika vikundi vidogo  vidogo vya ufugaji mkoani hapa  lengo  kuwanyanyua wafugaji hao kiuchumi ,hawakutaka kuwatumia madalali katika minada  ambao wamekuwa wakiwapunja wafugaji na kujinufaisha wenyewe  hivyo wameona watumie mwanya wa vikundi nao wapate faida kubwa na kuondokana na unyonywaji.


“Kiwanda hiki kinauwezo kwa kuchinja ng’ombe 250 hadi 300 kwa siku ila kwa kuanza tutaanzia ng’ombe 50 pia tumekwisha ongea na wasambazaji  kwenye masoko wa nyama hiyo pindi itakapo kuwa tayari,tumeongea na nchi ya uarabuni  wamedai wako tayari kununua  nyama yote  inayotoka ndani ya kiwanda hiki ikiwa tangu mwaka 2008  nimekuwa nikikifanyia ukarabati sasa kuanza rasmi ni mwezi Marchi mwaka huu.”alisema Self. 

Naye waziri Kamani alisema kuwa lengo la kuwepo kiwanda hicho nikutaka watanzania kuacha kuagiza bidhaa hiyo kutoka nje  na pindi kitakapo kuwa tayari  kitawezesha hata mikoa mingine  kuleta mifugo  yao ambapo barani Afrika  Tanzania imeonekana kuwa na mifugo mingi zaidi ya millioni  40  ikiwemo mbuzi na kondoo.

Aliwataka wafugaji watumie kiwanda cha nyumbani  kinachoweza kuchukua mifugo , ila changamoto kubwa iliyopo ng’ombe wa hapa nchini hawana ubora  wa kuingia kwenye ushindani wa soko la nyama hivyo inatakiwa wafugaji wabadilike kwa mfumo wa ufugaji na kuwa wa kibiashara  ili waweze kunyanyua uchumi wa mkoa  na mtu mmoja mmoja.

 Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Annarose Nyamubi alimtaka mwekezaji huyo kuwaelimisha wananchi  walio kandokando ya kiwanda hicho kwa kupitia afisa maendeleo  ya jamii kwa kutenga  maeneo ya kuendeleza shughuli zao ili kuweza kuepusha migogoro isiyokuwa yalazima pia wafugaji wapate kuelimishwa ili waweze kunufaika na kiwanda hicho.

Wafugaji kutoka  kata ya Samuye  wilayani humo  Mhoja Masengwa alisema kuwa  kiwanda hicho kabla ya kuanza kununua mifugo kwa wakulima watoe elimu ya mifugo gani wanayohitaji kama inakubalika waweze kuingia katika soko  isije badaye ikaonekana kuwanyima kipaumbele  wenyeji na kujikita katika wafugaji kutoka nje na kuonekana ndio wenye ubora zaidi.

Historia ya kiwanda hicho kilijengwa mwaka 1975  hakikuwahi kufanya kazi hata siku moja  ambapo mwaka wa 2008 kiliweza kupata mwekezaji  kutoka kampuni hiyo na kuanza kukifanyia ukarabati  wa kuondoa vifaa vilivyokuwa chakavu ikiwa  kinatarajiwa kuweka historia mkoani Shinyanga kwa kuanza kazi marchi mwaka huu.


0 Response to "KIWANDA CHA KUSINDIKA NYAMA CHAANZA MAZUNGUMZO NA WAFUGAJI KWENYE VIKUNDII"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.