Habari za hivi Punde

WAFUGAJI WILAYANI KISHAPU WATAKIWA KUBADILISHA MFUMO WA UFUGAJI KUTOKANA NA HALI YA HEWA KUWA YA UKAME




.
WAFUGAJI wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wametakiwa  kubadilika kufuga mifugo wenye uwezo wa kuchukua muda mfupi wa kukomaa na kuweza kuingia sokoni, pia kulichukulia kama zao la biashara  kutokana na hali ya hewa ya ukame katika wilaya hiyo  ikiwemo changamoto ya kukosa   maeneo ya malisho  pamoja na majosho.

Hayo yalisemwa na waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi  Titus Kamani  katika ziara yake aliyotembelea wilayani humo huku akiwaeleza wataalamu na mkuu wa wilaya hiyo Wilson Nkhambaku kuwa wakulima wamekuwa wakilima kila eneo na kufanya wafugaji kukosa maeneo ambapo inatakiwa wapatiwe elimu hiyo na kuweza kuepusha migogoro inayoendelea kati ya wakulima na wafugaji nchini.


Kamani alisema kuwa wafugaji wamekuwa wakikumbwa na changamoto nyingi  ya kufuga mifugo mingi yenye kuchukua muda mrefu kukua na kuingia sokoni  ambapo kumekuwa na uhaba wa meneo ya malisho kwao huku akisikitishwa na taarifa ya mkuu wa wilaya hiyo kuwepo kwa majosho 27 ila yanayofanya kazi ni majosho matatu.

“Wafugaji lazima wabadilike  wanauwezo wa kufuga mifugo  yenye kukomaa kwa muda wa  mwaka mmoja na nusu huku mbuzi akiweza kukomaa kwa muda wa miezi sita na kuingia katika soko la biashara, na kuichukulia kama zao  lao kuu kulingana na hali ya hewa ya ukame kwa mazao mengine kushindwa kustawi vizuri”alisema  Waziri  Kamani

Alisema kuwa sekta ya mifugo imekuwa haionekani kuingizia taifa pato la kutosha kama madini  ikiwa barani Afrika nchi ya Tanzania inaongoza kwa kuwa na mifugo mingi zaidi ya millioni  20, mbuzi millioni 15 na kondoo ni millioni 7   ambapo sekta  hii imekuwa ikilalamikiwa ,wafugaji  wamekata tamaa na kujichungia wanavyotaka  bila kujikita kuboresha suala hili,  hakika umasikini hauta ondoka.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo Nkhambaku  alibainisha kuwa asilimia 88.1 ya wakazi wa wilaya hiyo wanategemea uchumi wa kutoka kwenye kilimo na mifugo ikiwa asilimia 27  wanajihusisha na mifugo pekee ambapo kumekuwepo na ongezeko la mifugo isiyokuwa na tija kwa mwaka 2007 kulikuwa na ng’ombe zaidi ya laki mbili  na mikakati iliyopo ni uhimilishaji madume na majosho yaliyopo 27 yanayofanya kazi ni matatu.

Ambapo alisema kuwa kupitia uhimilishaji madume kwa mwaka 2012  kwa ng’ombe 200 na kuweza kupata ndama  zaidi  ya 10 katika vijiji sita ikiwa imetenga shilingi millioni 16 kwa lengo la kukarabati majosho 10 na shilingi millioni 71 kwaajili ya kununua madume bora 100 na kuamua kubadilisha mfumo wa ufugaji pia changamoto ya hali ya hewa  ukame  kwa kupata mvua wastani Mm 506 hadi Mm 567 na uhaba wa maji.

“Wilaya hii imekuwa na migogoro ya ardhi na mipaka kutoka kwa wakulima na wafugaji hasa kwenye vijiji vya Buzinza na Maghalata  pia mgogoro mwingine ni kati ya wilaya ya Kishapu  na Igunga,pia kumekuwepo na uhimilishaji wa ng’ombe 200 katika vijiji vitano na Majosho kwenye vijiji sita mikakati iliyopo majosho kumi kukarabatiwa  na kubadilisha mfumo wa ufugaji ili waweze kunufaika wafugaji”alisema Nkhambaku. 
  
Hata hivyo baadhi ya wafugaji  wilayani humo akiwemo  Jilunde Ndalu  alisema kuwa changamoto kubwa imekuwa ya uhaba wa maji  na malisho hali inayowafanya kuhama hama kwa kutafuta maeneo pia mifugo imekuwa na afya dhaifu kwa kukosa malisho hasa  kipindi cha kiangazi angalau  masika nyasi zinakuwepo mbugani  na  unafuu wa malisho kiasi.


0 Response to "WAFUGAJI WILAYANI KISHAPU WATAKIWA KUBADILISHA MFUMO WA UFUGAJI KUTOKANA NA HALI YA HEWA KUWA YA UKAME"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.