Habari za hivi Punde

UVCCM MANISPAA YA SHINYANGA WAIBUKA SHEREHE ZA KUADHIMISHA MIAKA 37 KUSAIDIA WATOTO WALEMAVU




KITUO  cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino) kilichopo Buhangija katika manispaa ya Shinyanga bado kinakabiliwa na upungufu mkubwa wa  chakula,  vyandarua,vifaa vya kufanyia usafi pamoja na upungugufu wa vitanda ambapo kuna watoto 258 huku kukiwa na vitanda 60.

Hali hiyo ya ukosefu wa vitanda imewalazimu kulala kila kitanda watoto wanne wanne ambavyo pia ni vitanda vya dable deca vinavyofaa kulaliwa na watoto wawili tu.

Hayo yalibainishwa juzi kwenye sherehe za kutimiza miaka 37 ya Chama cha mapinduzi (CCM) wakati umoja wa vijana UVCCM wilaya ya Shinyanga mjini  walipokuwa  wakiazimisha sherehe hiyo katika kituo hicho ambapo walifanya usafi katika maeneo hayo walifua nguo za watoto hao, walipanda miti pamoja na kutoa msaada wa chakula.


Akizungumza katika sherehe hiyo mkuu wa kituo hicho Britoni Mduma alisema bado wanakabiliwa na changamoto kubwa ya chakula kwani sasa hivi wana mahindi tu lakini hawana mboga, maharagwe mafuta pamoja na chakula cha kubadilisha.

“Vijana hawa wanakula chakula cha mlo mmoja tu ambacho ni ugali mchana na jioni kwa sababu hatuna chakula cha kuwabadilishia hivyo tunaiomba serikali iwakumbuke watoto hawa, pamoja na wahisani wengine mbalimbali waguswe  ili na wenyewe waweze kubadilisha chakula pamoja na kuwaongezea vitanda kwani wanalala kwa kubanana sana”alisema Mduma.

Kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa vijana UVCCM wilaya ya Shinyanga mjini Abubakari Mkadam alisema kuwa wameona vyema kuazimisha sherehe hizo za miaka 37 ya CCM kwa kutembelea katika kituo hicho kwa kuwasaidia kufanya usafi wa mazingira, kupanda miti kufua nguo pamoja na kutoa msaada wa chakula ,kwa lengo la kushiriki nao sherehe hizo za kuzaliwa kwa CCM.

Aliongeza kuwa sherehe nyingi za CCM zimekuwa ziki adhimishwa kwa kufanya mikutano mbalimbali ya wananchi ambapo kwa mwaka huu (2014) wameona wafanye tofauti kwa kuwa tembelea vijana wenzao ambao huishi katika mazingira magumu na hatarishi

Naye mjumbe wa Halmashauli kuu ya umoja wa vijana CCM  wilaya Lucas Jeremia alisema kuwa jamii inapaswa kutambua uwepo wa watoto hao kwani wanaishi maisha ya tabu sana na yamashaka hivyo inatikiwa kuwakumbuka kwa kuwapa misaada mbalimbali 

Aidha mmoja wa watoto hao walemavu wa ngozi Semen Deusi aliwashukuru vijana hao wa UVCCM kuwatembela katika kituo hicho na kukishukulu chama tawala kwa kuwakumbuka katika siku za maadhimisho yake huku akitoa wito kwa vyama vingine kuiga mfano huo

“Tunashukuru chama cha umoja wa vijana CCM kuja kuazimisha sherehe katika kituo chetu kwani haijawahi kutokea na tunaomba waendelee kufanya hivyo hata katika sherehe zingine pamoja na taasisi binafsi kwa kutusaidia licha ya kumaliza matatizo yetu hata kutupunguzia tu inatosha” alisema Mtoto huyo mlemavu

0 Response to "UVCCM MANISPAA YA SHINYANGA WAIBUKA SHEREHE ZA KUADHIMISHA MIAKA 37 KUSAIDIA WATOTO WALEMAVU"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.