Habari za hivi Punde

MADIWANI WA CHADEMA MANISPAA YA SHINYANGA WAJIUZURU NYASIFA HIZO




MADIWANI wawili wa chama cha maendeleo chadema  wametamka rasmi kujiuzuru nyasifa hiyo kutokana na madai ya uongozi ngazi ya taifa  kuendelea kusikiliza majungu,kudhalilisha baadhi ya viongozi  pamoja na  kuwaita  wahaini au wasaliti katika chama  bila kuchambua ukweli na kutotekeleza waliyoyaahidi kwa wanachama wao.


 Madiwani hao ni Sebastiani Peter  kutoka kata ya Ngokolo na Zacharia Mfuko kutoka kata ya Masekelo kwa pamoja jana waliongea na waandishi wa habari katika ofisi ya naibu meya wa manispaa hiyo huku wakieleza kuwa  wanayatamka rasmi maneno  mbalimbali yaliyopelekea kujiuzuru kama inshara ya kuwajibika kwa niaba ya makosa yaliyofanywa na viongozi wa kitaifa kwa nyakati tofauti.

Ambapo diwani Sebastiani alisema kuwa kuna sababu tatu zilizopelekea yeye kujiuzuru nafasi ya udiwani na ukatibu wa mbunge vita maalumu , ya kwanza ni mwezi Novemba  mwaka 2013 kikundi cha Briged kiliweza kuandika  barua kwa katibu mkuu wa chama hicho taifa na kulenga kuwadhalilisha  viongozi  akiwemo katibu  mkoa na wilaya kuwa wamehongwa kiasi cha shilling millioni  90.

“Tuhuma hii  leo ninaamini ni tuhuma ya uongo iliyolenga kuwadhalilisha viongozi  ambao ni Nyangaki Shilungusheila katibu wa mkoa na Siri yasini mwenyekiti wa wilaya  ambapo kimsingi  ndio walipotufikisha  hapa tulipo,kitendo cha katibu mkuu wa chama kupokea  barua hiyo na kushindwa kuifanyia kazi  wakati viongozi hawa  wamewahi kufungiwa  hata kwenye mkutano mkuu wa wilaya jambo hili limenifanya  niamini nyumba ya red brigedia  wapo viongozi  wa kitaifa  wanaowaagiza kufanya hayo”alisema diwani Sebastiani Peter.

Alisema jambo la pili ni kutokana na ahadi za mwenyekiti wa taifa Freeman Mbowe kuahihdi chama kitamaliza kujenga nyumba ya marehemu Shelembi  aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini na diwani kata ya Masekelo ambapo ahadi aliitoa siku ya mwisho  kwenye mazishi ya kiongozi huyo  katika viwanja vya shy-com huku mwenyekiti huyo katika kikao kingine alichokuwa akikiongoza kupinga ujenzi wa nyumba hiyo.


Jambo la tatu alisema kuwa tabia ya iliyozuka ndani ya chama hicho ni kuwaita baadhi ya  wanachama na viongozi  ikiwa ni pamoja kuwadhalilisha kwa kuwabatiza majina mbalimbali ya  wasaliti au wahaini wa chama ,waasisi wa kauli hizo  ni viongozi  hawa wa kitaifa kitendo kinachomfanya aamini kuwa ni uongo ambao hauna tija katika chama.

“Mimi ni miongoni mwa wanachama nitakao kuwa wa mwisho kuamini kama kweli mh Zitto Kabwe ,Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba  na wengine ni wasaliti ndani ya chama hiki binafsi najiuliza  kama kweli Zitto ni msaliti wa chama  na kwa mujibu wa taarifa  ya chama zinasema kuwa kutoka mwaka 2008 hadi 2009 aligundulika na kutumiwa na chama cha Mapinduzi (CCM)  swali mbona mwaka 2010  waliwezaje kumruhusu kugombea ubunge katika jimbo la Kigoma Kasikazini ?”alisema Sebastian Peter.


Alisema kwa hiari yake  kulingana na hayo aliyoyapima  ndani ya kichwa chake ameona kuna umuhimu wa kujiuzuru nafasi ya udiwani na ukatibu wa mbunge  ikiwa ni njia  ya kuwafundisha viongozi namna bora ya kuwajibika  kuliko kujionesha  mbele ya wananchi kwa mavazi ya kondoo wakati ndani ya mioyo ni mbwa mwitupia sijawa na mpango wa kujiunga na chama chochote nitabaki kuwa katika chama hicho.

Naye diwani wa kata ya Masekelo  Zacharia mfuko aliungana na diwani huyo kwa maelezo yake huku akisema kuwa uamuzi wake mpaka kujiuzulu ni kutokana na kuwepo  ubabaisha ji ndani ya chama hicho  kwani  lilikuwepo sakata la  mweyekiti wa mtaa  kukigawa kiwanja  huku kukiwa na kamati ya ugawaji alipokieleza chama walidai kukishughulikia lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea  na uongozi wa chama wamekaa kimya ikiwa kimeonekana dhahiri  kupingana na sera ya chama hicho kwa kuwatetea wanyonge.

Wote kwa pamoja walikabidhi barua zao  za kujiudhuru udiwani  katika ofisi za manispaa huku wakimueleza kaimu mkurugenzi Mwanamsiu Dossi  taarifa  juu ya uamuzi waliouchukua,kuwaombea radhi  kama sehemu waliokwaruzana na  watendaji wote waliokuwa wakifanya nao kazi  kwa pamoja  ambapo waliwataka wananchi wa kata zote kuwaona kuwa kitendo walichokifanya sio kwa nia mbaya bali kulijenga taifa  lililo makini.

 K wa kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010  manispaa hiyo  ilipata madiwani kumi na saba ambapo chama cha Mapinduzi kilikuwa na madiwani kumi na nne huku chama cha chadema  kikiwa na madiwani   wanane

0 Response to "MADIWANI WA CHADEMA MANISPAA YA SHINYANGA WAJIUZURU NYASIFA HIZO"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.