Habari za hivi Punde

TANESCO MIKOA YA SIMIYU NA SHINYANGA YAWAONYA VISHOKA WANAOHARIBU MIUNDOMBINU





SHIRIKA la umeme Tanzania (TANESCO) katika mikoa ya simiyu na shinyanga limewaonya  wale wote watakao haribu miundo mbinu ya shirika hilo  wakiwemo  vishoka ambao wamekuwa wakililetea shirika hasara kubwa  kwa kuharibu mita na kufanya gharama za uzalishaji na uendeshaji kuwa kubwa hivyo watakao bainika  kwa uhalibifu  huo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Hayo yalibainishwa mjini shinyanga kwenye mkutano wa hadhara na Afisa mkuu wa huduma kwa wateja TANESCO katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga Musa Kasimu wakati akitoa elimu kwa wakazi wa mjini humo  juu ya huduma zinazotolewa na shirika la TANESCO  kwa wananchi


Kasimu alisema  baadhi ya wananchi katika mikoa hiyo miwili wamekuwa na tabia ya kuharibu miundo mbinu ya shirika hilo huku wengine wakishirikiana na vishoka kuharibu vifaa hivyo hasa kwa upande wa Meter na Luku ambavyo mara kwa mara vimekuwa vikichokonolewa kwa lengo la kupunguza gharama za umeme

Alisema vitendo hivyo vinafaa kukemewa kwa nguvu zote kwani kufanya hivyo ni kuhujumu miundombinu ya shirika hilo na uchumi wa nchi ikiwa ni pamoja na kusababisha hitilafu katika vifaa hivyo vya umeme “METER” NA “LUKU”  hali ambayo husababisha kuongezeka kwa bili za umeme tofauti na matumizi.

Naye  Afisa uhusiano wa shirika hilo katika mikoa ya shinyanga na Simiyu  Amosi Michael alikiri kuwepo kwa baadhi ya vishoka kutoka ndani ya shirika hilo mara baada ya kuulizwa ni watu gani ambao wamekuwa wakishirikiana na baadhi ya wateja  kuharibu miundombinu  kwa lengo la kukwepa gharama.

‘Nikweli kuna baadhi ya vishoka wanatoka ndani ya shirika letu kushiriki na wananchi kufanya shughuli za kuharibu miundo mbinu ,kwani mtu anayefanya kazi hiyo lazima awe na ujuzi na tunapo wabaini kuhusika na vitendo hivyo tunawafukuza kazi ,na upande wa wananchi tunawatoza faini lakini katika kipindi hiki ni mahakamani tu” alieleza Michael

 Afisa usalama washirika la TANESCO kutoka mikoa hiyo miwili Kenedi Peter aliwataka wakulima wa mikoa hiyo ya Shinyanga na Simiyu kuacha tabia ya kulima mazao karibu na nguzo za umeme  kitendo ambacho husababisha nguzo kuanguka na kutokea katizo la umeme kutokana na kufanya marekebisho ya nguzo hizo.

 Pia alisema Shirika hilo hivi karibuni limetoa elimu mkoani Simiyu katika vijiji 15 kutoka katika wilaya za Meatu, Maswa ,Bariadi, na Itilima huku katika mkoa wa Shinyanga elimu hiyo ikitolewa katika vijiji vya Salawe, miganha pamoja na mjini shinyanga

0 Response to "TANESCO MIKOA YA SIMIYU NA SHINYANGA YAWAONYA VISHOKA WANAOHARIBU MIUNDOMBINU"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.