Habari za hivi Punde

MADIWANI WALIOJIUZURU NA KUJIVUA UANACHAMA CHADEMA WAJIUNGA NA CCM MKOANI SHINYANGA




MADIWANI waliojiuzuru  nyasifa hiyo na kuamua kuondoka  katika chama cha CHADEMA  ambao ni  Sebastiani  Peter na Zacharia Mfuko  wamejiunga rasmi  na chama cha Mapinduzi  (CCM) mbele ya katibu wa itikadi na uenezi Nape Nnauye na uongozi wa mkoa wa chama hicho.

Maelfu ya wakazi  wa mkoa wa Shinyanga wakihudhuria mkutano wa hadhara  uliofanyika katika viwanja  vya  Mahakama Nguzo nane  huku wakishuhudia waliokuwa wananchama  na viongozi ndani ya Chadema wakipanda jukwaani ghafla huku wakiwa wamevaa kofia za CCM na kueleza kiliwafanya kujiunga na chama hicho  kutokana na kutuhumiwa kila kukicha kuwa ni mamluki ndani ya Chadema.


Madiwani hao walisema kwa nyakati tofauti huku wakiwa wamepanda katika jukwaa  na kuwaeleza wananchi kuwa wasione ajabu  kuwa ndani ya CCM  kwani wamekuwa wakituhumiwa  kutumika na chama hicho pale wanapofanya vizuri na kupinga yasiyo halali hivyo hawawezi kuwa na chama ambacho hakina utaratibu  na utovu wa nidhamu.

“Wananchi wa kata yangu ni mashuhuda walinichagua masikini sina hata uwanja na sasa nimeamua kuondoka ndani ya chadema,  ni miongoni mwa madiwani manispaa nilofanya vizuri kwa kutekeleza ahadi yangu,naondoka  yanabaki majungu kuwa nimenunuliwa lakini ningejiunga  na chadema natoka CCM wangeniita komando  wanayoyasema hayo wote ni mbumbu wa  mawazo”alisema  diwani aliyejiuzuru chadema  kutoka kata ya Ngokolo Peter.

Diwani wa kata ya Masekelo  Mfuko alisema kuwa mara baada ya kutoa taarifa katika vyombo vya habari   amekuwa akipata ujumbe katika simu yake ya mkononi  ya  vitisho huku  akidaiwa kupewa fedha   na chama cha mapinduzi  jambo ambalo linamshangaza kwani kila mmoja anauhuru wa kuamua  aende chama gani kitakacho mfaa.

Naye Nape Nnauye katika mkutano huo aliwapokea kwa shangwe  wanachama hao kwa kuwapatia kadi za  CCM huku akisema kuwa vijana wanatakiwa wasifukuzwe katika vyama  kwani ndio nguzo inayofanya kuwepo kwa mabadiliko nchini,akitolea mfano wa Mh Zitto Kabwe aliingia  chadema akiwa na umri wa miaka 16  lakini sasa wanamwita msaliti ingawa ameitengeneza chama hicho na kusimama imara.

Hata hivyo madiwani hao  wawili ambao wanatoka katika kata za Masekelo na Ngokolo walijiuzuru ndani ya wiki hii  huku wakitoa sababu mbalimbli za kutofurahishwa na mienendo mibaya ndani ya chadema  kwa viongozi wa kitaifa kuwadhalilisha  viongozi wa mkoani Shinyanga huku wakiacha kutekeleza waliokuwa wakiyaahidi.

0 Response to "MADIWANI WALIOJIUZURU NA KUJIVUA UANACHAMA CHADEMA WAJIUNGA NA CCM MKOANI SHINYANGA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.