Habari za hivi Punde

MAHAKAMA KUU KANDA YA TABORA YAANZA KUSIKILIZA KESI ZA MAUAJI MKOANI SHINYANGA NA SIMIYU.

MAHAKAMA  kuu kanda ya Tabora imeanza kusikiliza kesi za mauaji  mbalimbali katika mkoa wa Shinyanga kwa mwaka huu ikiwa kesi kumi na moja  zitasikilizwa ndani ya mwezi mmoja ikiwemo  mauaji yanayotokana na imani za kishirikina.

Ambapo mara baada ya kumalizika ufunguzi wa kusikiliza kesi hizo mahakama  ilianza  kwa kuangalia upande wa  mtuhumiwa Mbula  Mako aliyekuwa mganga wa kienyeji  kufanya mauaji  dhidi ya kikongwe Buguta Mashilima huko katika kijiji cha Nobora wilayani Bariadi mkoani Simiyu.



Kesi hiyo iliendeshwa na    jaji Haruna Songoro huku akisema kuwa  mkoa wa Shinyanga na Simiyu unakesi nyingi ambapo  jumla ya kesi 11 za mauaji zitasikilizwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Katika ufunguzi uliozinduliwa na jaji Songoro kwa kusikiliza  kesi za mauaji mbalimbali Siku ya kwanza ya  kuendesha kikao kulifanyika usikilizwaji  wa  kesi moja ya mauaji yaliodaiwa kutokea kwa imani potofu za ushirikina.

Kwa  upande wa mashitaka  mtuhumiwa alitenda mauaji hayo mnamo novemba  21 ,2011 kijiji cha nobora bariadi majira ya usiku baada ya kumtumbikiza  kisimani marehemu ambaye alikuwa bibi yake.



Hata hivyo  changamoto kubwa katika mahakama ya mkoa wa Shinyanga imedaiwa kuwepo mrundikano wa kesi mbalimbali zikiwemo za mauaji  ya vikongwe kwa imani za kishirikina ambazo hazijasikilizwa na kutolewa hukumu.

Naye hakimu mkazi mwandamizi mfawidhi mkoa wa shinyanga John Meseka Chaba ameiomba serikali hapa nchini kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa shinyanga kukamilisha ujenzi wa jengo la mahakama kuu kanda ya ziwa linalojengwa mkoani hapa ilikurahisisha uendeshaji wa kesi hali ambayo itasaidia kesi nyingi kusikilzwa kwa wakati

“Endapo jengo la mahakama ya Rufaa kanda ya ziwa mkoani hapa litakapokamilika litasaidia kuepusha mrundikano wa kesi mahakamani kwani kesi nyingi hupangiwa tarehe kila mara kutokana na uhaba wa majengo ya mahakama kuendeshea kesi hizo pamoja na upungufu wa mahakimu kwani kesi nyingine zinakuwa hazijamaliza upelelezi”alisema Chaba








0 Response to "MAHAKAMA KUU KANDA YA TABORA YAANZA KUSIKILIZA KESI ZA MAUAJI MKOANI SHINYANGA NA SIMIYU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.