Habari za hivi Punde

VIJANA KUTOJITAMBUA WAMESHINDWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA MCHAKATO WA KUTOA MAWAZO YAO RASMU YA KATIBA MPYA

KITENDO cha vijana kutokujitambua  kumesababisha washindwe kushiriki kikamilifu katika  mchakato wa kutoa mawazo yao kuhusu rasmu ya katiba mpya.
Hayo yalielezwa na Mkurungenzi wa Asasi  isiyo ya kiserikali inayotetea haki za wanawake na  watoto wenye maambukizi ya virusi  vinavyosababisha  Ukimwi  (AGAPE)   John  Myolla   katika ufunguzi   wa kongamano la vijana kujadili rasmu ya katiba mpya lililofanyika mjini hapa  jana.
Myolla alisema  kundi la vijana lina umuhimu wa pekee kwa jamii, lakini wameshindwa kujitambua  na kujikuta wakijishughulisha na mambo  ya  mzaha na kupuuza  yale  yenye  kuleta tija kwa taifa.
Alisema idadi kubwa ya vijana haikujitokeza kushiriki katika mikutano ya kujadili na kutoa mapendekezo yao  na kueleza wangelipenda  katiba mpya  itaje mambo yapi yatakayowasaidia vijana nchini.
“Vijana wengi  nchini hawakujitokeza kwenye mikutano ya kujadili  rasmu ya katiba mpya kwa kisingizio cha kukosa nafasi  ya  kwenda kushiriki  katika  mikutano hiyo na badala yake walikwenda  kwenye viwanja  vya  michezo na kumbi za   Mziki”      alisema Myolla.
Alisema kuwa ukitaka kupima ushiriki wa vijana katika mikutano ya kujadili rasmu ya katiba mpya tazama rasmu ya katiba sura ya nne sehemu ya kwanza ya Ibara ya 44 inayozungumzia haki na wajibu wa vijana zimeandikwa  senteso mbili pekee hiyo ni kudhihirisha kuwa vijana hawakutoa mapendekezo yao katiba mpya  iwe ya ainagani.
Naye kijana Nyangata Sungura mkazi wa kitongoji cha Ndala, Manispaa ya Shinyanga alisema vijana hawapaswi  kuilalamikia serikali kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo  ukosefu wa ajira kutokana na kupuuza mipango muhimu.
Kwa upande wake mwezeshaji na mtoa mada wa kujitolea kutoka katika Shirika lisilo la kiserikali la Restless  Develoment   (RDT) John   Eddy alisema licha ya vijana kushindwa kutoa mawazo yao kuhusu rasmu ya katiba mpya,  hata hivyo aliwashauri kuisoma  rasmu ya katiba mpya  kwa lengo la kubaini maeneo yalio  na upungufu  na kutoa mawazo  yao yanayohusu  kupata  katiba inayokidhi haja.
 
 
 
 
 

0 Response to "VIJANA KUTOJITAMBUA WAMESHINDWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA MCHAKATO WA KUTOA MAWAZO YAO RASMU YA KATIBA MPYA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.