Habari za hivi Punde

SHULE YA SEKONDARI MASEKELO INAKABILIWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI IKIWEMO UKOSEFU WA VIWANJA VYA MICHEZO,UHABA WA MAJI PAMOJA NA MASHAMBA

SHULE ya sekondari   Masekelo iliyopo kwenye kata hiyo manispaa ya Shinyanga  inakabiliwa na changamoto mbalimbali  ya kukosa eneo kwaajili viwanja vya michezo, mashamba ya kulima vyakula ,uhaba wa maji , hali ambayo inawafanya  wanafunzi wa shule hiyo kukosa haki zao za msingi.

Zoezi la utekelezaji kilimo cha mtama kwa shule hiyo halipo sababu ya kukosa mashamba,hakuna eneo lililotengwa  viwanja vya michezo ikiwa wananchi wanalima mpaka nyuma ya madarasa ya shule  huku bado wenye mashamba yao walionyang’anywa na manispaa hawajalipwa fidia,pia haina maji ingawa wanapata uji wanafunzi shuleni hapo kwa kulipia shilingi  40,000 kwa mwaka.

 Mkuu wa shule hiyo  Stephen Mihambo  aliongea na baadhi ya  waandishi wa habari waliotembelea shuleni hapo  huku akieleza kuwa shule  inajumla ya wanafunzi  319 ,vipindi vya michezo vipo ila hakuna uwanja wa michezo, hali inayojionyesha ni mwamko mdogo wa jamii katika suala zima la elimu  kwa kushindwa kutoa maeneo ya mashamba yao ili shule ipate viwanja vya michezo.

“Katika suala la maji lilifanyiwa makadirio mwaka 2012  kwa kuishirikisha mamlaka ya maji safi na mazingira  (Shuwasa), ili yapatikane maji  ya bomba kwakuhitajika zaidi ya shilingi  millioni 28, ila kwa sasa linafanyiwa mchakato  na kuahidiwa katika  fedha za mfuko wa jimbo suala hilo litatekelezwa ila kwa sasa maji yanayopatikana  shuleni hapo  huwapatia tenda watu na kutofahamu  yanatolewa wapi salama au si salama”.alisema   Mihambo.

Ambapo alisema  kilimo cha mtama shuleni hapo kutokana na kampeni inayofanywa na serikali ya mkoa kuwa kila shule ilime angalau ekari mbili za mtama kimeshindikana ili kupatikane chakula , sababu ya kukosa mashamba ya kulima ili kuweza kupunguza tatizo la uchangishwaji fedha kwa wazazi kwaajili ya uji au chakula cha mchana.

Kaimu afisa mtendaji wa kata hiyo Ester Daudi alisema kuwa  suala zima la changamoto hizo kweli ila kwa upande wa mashamba  wananchi bado hawajalipwa fidia  ambapo  liliwasilishwa manispaa,suala la uhaba wa maji kwa kukosa mabomba lipo na lilijadiliwa  mara baada ya kupokea barua ya uthibitisho wa fedha za jimbo  tayari kumependekezwa kutekeleza upatikanaji wa maji ya bomba shuleni hapo.

Naye diwani wa kata hiyo Zacharia Mfuko alikiri kuwepo kwa changamoto hizo shuleni hapo huku akisema kuwa  tangu mwaka wa 2012 suala hilo limeanza kuzungumziwa  katika manispaa na mchakato bado unaendelea ila maji yanayopatikana kwa sasa katika shule hutoka sehemu mbalimbali nje ya kata hiyo hali ambayo inaonyesha hata kuhatarisha afya za watumiaji.

Alisema kuwa mashamba hayo  wananchi bado hawajalipwa fidia tangu mwaka 2007,ikiwa  suala hilo  mpaka sasa lipo kwenye ofisi ya mipango miji na linafanyiwa kazi  pamoja na hayo shule kweli inatatizo la ukosefu wa uwanja wa michezo  naye  mwenyekiti wa bodi  ya shule  hiyo Deogratius Shitenge alikiri kuwepo kwa changamoto hizo huku akieleza kuwa vikao vimekaa na kuahidi kuyatekeleza ikiwa fedha zitapatikana.

Baadhi ya wananchi wa kata hiyo akiwemo  Monica Ndalu na Kwilasa Mahene  walisema kuwa maeneo yao yalichukuliwa kwa lengo la kupisha ujenzi wa shule lakini mpaka sasa bado  hawajalipwa fidia ambapo sehemu ya mashamba yaliyokaribu na shule hiyo wanalazimika kuyaendeleza  kwa kukosa maeneo mbadala kwaajili ya kilimo .

0 Response to "SHULE YA SEKONDARI MASEKELO INAKABILIWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI IKIWEMO UKOSEFU WA VIWANJA VYA MICHEZO,UHABA WA MAJI PAMOJA NA MASHAMBA"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.