Habari za hivi Punde

UKATILI WA KIJINSIA KATIKA JAMII UNALETWA NA MTAZAMO HASI





UKATILI wa kijinsia  katika jamii na familia   unaletwa  na mtazamo hasi  kwani  matendo kati ya mwanamke na mwanaume  yanategemeana  ambapo  mifarakano hutokea kwa kupingana na kuendeleza changamoto zilizomo kwenye mila na desturi   ikiwemo kuwazuia watoto wa kike  kupata elimu ,ndoa za utotoni   pamoja na ukeketwaji.

Hayo yalisemwa na mwezeshaji  ambaye ni pia ni mhariri mtendaji wa gazeti la jamhuri  Deogratius Balile kwenye semina iliyowajumuisha waandishi wa habari  kutoka mikoa ya Simiyu na Shinyanga yaliyoandaliwa na chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (Tamwa) huku  akieleza kuwa waandishi  wananafasi kubwa ya kuibadilisha jamii .


Balile alisema kuwa ukatili wa kijinsia unaletwa kwa mtazamo hasi ikiwa matendo kati ya mwanaume na mwanamke yanategemeana  hata katika uleaji watoto katika familia,hivyo waandishi wa habari hawana budi kuibadilisha jamii  kwa kutumia kalamu zao na jinsi matukio  na elimu inavyotolewa ndio jamii imeanza kupunguza vitendo vya ukatili hapa nchini.

Alisema  kwa hivi sasa wanawake  wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 35  takwimu zinaonyesha kuwa ni asilimia 39 waliokeketwa tayari huku  wenye umri wa miaka 17 hadi 24 takwimu hizo zinaonyesha pia waliokeketwa ni asilimia 10 inaonekana kadri  waandishi wa habari wanavyoripoti  elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia  kupitia vyombo vya habari jamii imeanza kuelewa   na matukio yamepungua.

Pia aliwataka  kuondoa dhana ya uandishi wa kiubaguzi  kwa kumtenganisha mtoto na mama katika matukio yanaporipotiwa kwenye vyombo vya habari  tofauti na wanavyoripoti  matukio kwa wanaume ambapo  kumejitokeza dosari ndogondogo nyingi zinazo onyesha kumtenga mwanamke asionekane  ana haki  ya kuwa katika nafasi mbalimbali au hata katika jambo lolote linapotokea.

“Waandishi wa habari mmekuwa mkiripoti matukio yanayotokea  kwa kumtenga mtoto na mama huku mkiwataja jinsia zao halafu  majina  yao yanafuata tofauti na wanaume hawatajwi   jinsia zao matokeao yake hutajwa majina hilo nalo limeonekana ni dosari kubwa katika uripotiwaji wake nakuona kama wanawake na watoto bado hawatendewi haki  kwenye vyombo vya habari”alisema  Balile.

Balile akizungumzia suala la  kutailiwa kwa wanaume  ambapo alidai  linaingizwa katika ukatili wa kijinsia  ingawa kwa hivi sasa serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii imeliunga mkono suala hilo kwa kuona linauwezo wa kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi katika jamii.

Aliwaeleza waandishi hao kuwa kitu cha kufanya sasa ni kusoma ili kuweza kujikomboa kiuchumi na  kuripoti vizuri  matukio yanayoendelea kutokea  kwa kuyapambanua kwa  kina  jinsi ukatili unavyofanywa katika jamii  na kuondoa  dosari zinazojitokeza pindi zinaporipotiwa  kwenye vyombo vya habari .

Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria semina hiyo akiwemo selemani Abeid na  Zulfa Mfinanga walieleza kuwa  ukatili bado unafanywa katika jamii japo umepungua hivyo kupitia mafunzo hayo watatekeleza kuziondoa dosari zilizoelezwa  wakati wa kuziripoti huku wakitaka mafunzo hayo yatolewe mara kwa mara kwa waandishi ili uelewa uwepo zaidi.

0 Response to "UKATILI WA KIJINSIA KATIKA JAMII UNALETWA NA MTAZAMO HASI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.