Habari za hivi Punde

WAUZAJI TINDIKALI WATAKIWA KUJISAJILI KATIKA OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI

JESHI la polisi mkoani Simiyu limewataka wauzaji wa tindikari mkoani humo  kuhakikisha wanasajiliwa na ofisi ya mkemia mkuu wa serikali, ili kutambulika kisheria sambamba na kupewa utaratibu wa matumizi sahihi ya bidhaa hiyo kwa lengo la kuondoa matumizi mabaya ikiwemo kuwadhuru watu.

Mbali na hilo kamanda  wa jeshi hilo Charles mkumbo amewatahadharisha wananchi wote ,kuwa kwa yeyote atakayekutwa na tindikari mtaani, atakamatwa, ikiwa pamoja na kufikishwa mahakani.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jana kamanda Mkumbo alisema kuwa katika utaraatibu uliowekwa kwa sasa kwa wauzaji wa bidhaa hiyo unamtaka kila muuza tindikari kusajiliwa na ofisi ya mkemia mkuu,sambamba na kupewa maelekezo ya jinsi ya kutumia au kuuza bidhaa hiyo.

Alisema kwa kila atakayehitaji tindikari kwa matumiuzi sahihi, atatakiwa kuja na mtu au kupewa kibali na mtu atakayetumia tindikari hiyo,kama kwenye magari au pikipiki atatakiwa kuja na fundi makenika dukani kuchukua bidhaa hiyo.
 
Katika utaratibu huu ambao ni mpya unao lenga kukomesha matukio ya kumwagiwa watu tindikari,utamtaka muuzaji wa bidhaa hiyo kuhakikisha kila anayenunua tindikari anaitumia katika matumizi sahihi  na  atakayeruhusiwa kutumia au kuja na kibali”alisema.

Alibanisha kuwa  baadhi ya maofisa kutoka ofisi ya mkemia mkuu kanda ya ziwa iliyoko Jijini Mwanza wamewasili mkoani hapa na watakuwepokwa siku kumi,ili kufanya usajili huo,sambamba na kutoa elimu pamoja na utaratibu wa juu ya matumizi ya tindikari.

Kamanda huyo alieleza  kuwa jeshi la polisi halitakuwa na huruma kwa yeyote atakaye kutwa na tindikari mtaani, kuwa atakatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria  huku akiwataka watumiaji wa bidhaa hiyo kufuata utaratibu huo mpya.

0 Response to "WAUZAJI TINDIKALI WATAKIWA KUJISAJILI KATIKA OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.