Habari za hivi Punde

ZAHANATI YAFUNGWA KWA KUKOSA VIGEZO.



ZAHANATI  inayomilikiwa na  mtu binafsi katika kijiji cha songambele kata ya Salawe wilayani Shinyanga  imefungwa na wataalamu  wa afya kutoka    mkoani  hapa  kutokana na kukosa vigezo  vya kuwa zahanati  babala  ya  duka la  madawa kama  ilivyokusudiwa  huku  daktari   msimamizi wa  wakimkataa kwa kukosa sifa,  ambapo  ilikuwa ikitoa huduma mbalimbali za matibabu  kama vile upimaji wa  damu,malaria  na uzalishaji wa mama wajawazito.

Zahanati hiyo imefungwa mwezi januari  mwaka huu,ambapo  mmiliki wake dkt Daniel Emanuel  aliwaeleza waandishi wa habari kuwa  zahanati imepata usajili  mwaka 1994 na kuanza kutoa huduma    katika kijiji hicho ambapo kwa siku  alikuwa akihudumia  wagonjwa zaidi ya  kumi.

Dkt  Emanuel  alisema    kuwa   haelewi sababu za kufungwa kwa zahanati hiyo  kwani walifika wataalamu wa afya kutoka  mkoani  na kumueleza kuwa  hana wataalamu wa kutosha kuendesha zahanati hiyo  huku  wakimkataa msimamizi wa  zahanati kuwa hana sifa  na  hakuna wataalamu wakutosha.

Ambapo ameeleza kuwa zahanati hiyo ilikuwa na wafanyakazi watano akiwemo msimamizi ambaye walimkataa kwa madai hana sifa ya kusimamia zahanati hiyo sanjari na kukagua vipimo vilivyomo ndani ya maabara huku wakiondoka na vifaa hivyo.

“Mimi nashangazwa na wataalamu  kutoka serikalini  kuja kunifungia  kwani wataalamu ninao wa watano , wakiwemo wauguzi  na daktari wenye sifa ,  kisheria  zahanati inatakiwa   hata wakiwa wawili  inatosha kwa sababu  huduma zinazotolewa  sio nyingi ,ila msimamizi wa  zahanati wamemkataa  kuwa hana sifa kipimo cha maabara wamekichukua na kuondoka nacho.”alisema  dkt Emanuel.

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho  Mhoja  Shija  na James Membe walisema  kuwa  zahanati hiyo ilikuwa msaada mkubwa kwa  watu ndani ya kijiji hicho  na kuwa kimbilio  mara  wanapougua kwa kupata huduma   ya haraka japo kwa  malipo  tofauti na zahanati  ya serikali  mara nyingi  zimekuwa na  changamoto nyingi  hasa za ukosefu wa  dawa .

Naye mwenyekiti wa halmashauri hiyo Ngassa Mboje alisema  kuwa kufungiwa kwa zahanati hiyo imetokana na kukosa sifa ikiwemo  kwenye orodha ya usajili kama  zahanati haimo ambapo inaonekana  mpaka sasa ni duka la uuzaji wa dawa na kutofuata utaratibu wa sheria za afya.

Mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya  hiyo dkt  Archie Hella  alisema   kufungiwa kwa  zahanati hiyo  kutokana na  kushindwa kufikia vigezo vya kuwa zahanati  ambapo ilibainika kuwa   haina  wataalamu wenye sifa  wa kuweza kutoa huduma hiyo kwa watu pia ilikuwa ikiendesha  kinyume cha sheria na taratibu za  afya.

 

0 Response to "ZAHANATI YAFUNGWA KWA KUKOSA VIGEZO."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.