Habari za hivi Punde

JAMII IMETAKIWA KUJIOMBEA NA KULIOMBEA TAIFA HASA KIPINDI HIKI CHA MCHAKATO WA KUUNDA KATIBA MPYA.




JAMII mkoani Shinyanga imetakiwa kujiombea  na kuliombea taifa katika mchakato huu wa  kuunda katiba mpya  kwenye msimu huu wa kumalizika  kwa mateso ya yesu kristo aliyejitoa  na kusulubiwa  msalabani kwaajili ya dhambi za wanadamu huku akiwataka kutenda yaliyo mema duniani.

Hayo  yalisemwa  jana  na  mchungaji  peter   Msengi   wa kanisa la Moravian lililopo Ngokolo kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga  katika ibada ya  siku ya ijumaa kuu mbele ya waumini wa kanisa hilo huku ikiwemo imani kutoka kwenye  kitabu cha maandiko kuwa  binadamu hana kosa  na kufikia hatua ya kukiri mwenyewe.


 Mchungaji Msengi alisema  kuwa  katika ibada  hiyo ujumbe uliotolewa, binadamu anaweza kubadilika  hivyo jamii imetakiwa kujiombea kutokana na changamoto  wanazokabiliana nazo ikiwemo kuliombea taifa  na mchakato unaoendelea  wa kuipata katiba mpya.

“Ninanukuu maandiko yesu alisema imekwisha maana yake alijitoa  sababu ya  dhambi  zetu baada ya kupata adhabu zote ikiwemo kutundikwa  msalabani  hatimaye alisema tena nimeshinda  akimaanisha  binadamu hata kusumbuka kwa magonjwa, shida na njaa”alisema  mchungaji Msengi.

Mchungaji  Msengi alisema  kuwa yesu kristo alikabidhi  roho yake  akimaanisha  maovu yote na dhambi zimekwisha kilichobaki ni binadamu kuendelea kutenda mema katika dunia.

Hata hivyo alisema  kuwa  binadamu wanatakiwa kutafakari  maneno ya mwisho ya mungu aliyonena kila binadamu anauwezo wa kuililia familia yake kutokana na  baadhi ya vitendo vya maudhi vinavyoibuka  na sio kumlilia aliyemkombozi wa wakristo yesu.

Wasiohudhuria  katika  ibada  siku zote   na kutegemea  siku maalumu kama za siku kuu alisema  hao wanatakiwa  kuombewa na kuwatia moyo ili  waweze kuhudhuria  wakati wote wa  ibada, binadamu anatakiwa  atende mema  duniani  na kufuata yaliyonenwa na mwokozi yesu kristo ikiwa kuliombea taifa na familia zao kwa ujumla.

0 Response to "JAMII IMETAKIWA KUJIOMBEA NA KULIOMBEA TAIFA HASA KIPINDI HIKI CHA MCHAKATO WA KUUNDA KATIBA MPYA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.