Habari za hivi Punde

MASHIRIKA YA UMMA YAPATA HASARA KUBWA KUTOKANA NA KUIBIWA KWA MIUNDOMBINU YAKE

CHANGAMOTO  inayowakumba mashirika ya umma nchini ni kuibiwa kwa miundombinu mbalimbali ya vifaa vinavyotumika kwenye ujenzi  wa miundombinu mbalimbali  ambapo  shirika la  umeme (TANESCO)  mkoani  Shinyanga limeeleza kupata hasara kiasi cha shilingi millioni 9.5 kwa  mwaka 2012 huku shirika la mawasiliano  mkoani Shinyanga (TTCL) likipata hasara ya  zaidi ya shilingi millioni 108.
Ambapo Shirika la Reli  (TRL) kwa  wizi wa Mataluma ya kwenye barabara wameeleza   kuwepo kwa biashara ya vyuma chakavu,kutumia  kwenye majembe yanayokokotwa na ng’ombe pamoja na shirika la mawasiliano nchini  TTCL wakieleza baadhi ya wakulima kuchimbua nyaya zilizopo ardhini zinazohusika kupita kwa mkongo  wa  mawasiliano wa Taifa.
  Hayo waliyasema kwenye mkutano wa   viongozi wa sungusungu   uliofanyika kwenye uwanja wa Kolandoto    katika kata hiyo    kwa kukutanisha   wilaya tatu za  Kishapu,  Manispaa na  Shinyanga  mkoani  hapa   huku ajenda kuu zikiwa mbili za ulinzi wa  miundombinu na  mahudhurio kwa wanafunzi mashuleni.
Ambapo ajenda  ya  ulinzi wa miundombinu  viongozi wa  mashirika hayo walianza kutoa ufafanuzi  mbele  ya  jeshi la sungusungu   namna gani wanavyopata hasara kutokana na miundombinu kuibiwa au kuharibiwa na jamii wasiopenda maendeleo ikiwa ofisa  mahusiano wa  shirika la umeme  Tanesco  Michael  Amon  alisema  shirika hilo limepoteza kiasi cha shilingi Billioni 3.5  kutokana na wizi wa nyanya  au vyuma katika  transfoma  pekee.
“Unapohujumu  miundombinu  ya  Tanesco   ni kuipatia nchi hasara kubwa  ikiwa uchumi unashuka ,mawasiliano yatakosekana  watoto watafeli  shule kutokana na kutegemea masomo  mengine nishati ya umeme hivyo viongozi wa sungusungu mnatakiwa kuwa mabalozi  kwa wananchi  kutoa elimu na kuwabaini wanaofanya uhalibifu huo lengo ni kujinufaisha kwa matumizi yao binafsi kisheria ni kosa”alisema  Amoni.
Naye mhandisi wa  Tanesco  Job Bidya  alisema  kuibiwa  kwa vipande  vya vyuma 107 kwenye laini inayopeleka umeme  Mgodi wa Bulyanhulu  gharama yake ni shilingi  millioni 9.5   ambayo serikali imeingia hasara hiyo  ikiwa mgodi huo ulikosa umeme kwa  siku 14 uliweza kupata hasara   kwenye  uzalishaji kiasi cha shilingi zaidi ya  billioni  14.
 Meneja wa  shirika la mawasiliano TTCL  mkoani Shinyanga  Peter  Kuguru alisema kuwa  miundombinu ya shirika hilo imekuwa ikiharibiwa hasa na wakulima wanaolima kando ya barabara palipochimbiwa nyaya zinazopita mkongo wa mawasiliano  wa  Taifa na kufanya  mawasiliano yakiwemo ya mitando kwenye maofisi,mabenki  hospitalini kushindwa kufanya kazi sababu kuu ikiwa ni uhalibifu.
Kuguru alisema kuwa  hujuma inayofanywa  na baadhi ya watu kukata nyaya  hizo bila kwenda kuifanyia shughuli yoyote  ikiwa   cable moja gharama yake zaidi ya shilingi millioni 10 kwa hasara inayopatikana,  ambapo mwezi  Novemba mwaka jana    hadi leo hii hasara iliyopatikana ni zaidi ya shilingi millioni 108.
Naye  mwakilishi  wa  shirika la reli  kutoka  mkoani  Mwanza  insp Suzan  Kidiku alisema kuwa  miundombinu ya  reli   ni jukumu la kila mwananchi kuilinda kwa kuwa ndio njia ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na abiria  ikiwa jamii imekuwa haitoi ushirikiano  wa kubaini wanaofanya uhalibifu huo huku wengine wakitumia kama spea  za kwenye majembe ya kukokotwa na ng’ombe na kupeleka kuuza katika biashara ya vyuma chakavu.
Baadhi ya viongozi wa sungusungu akiwemo Jackob  Charles  katibu  wa sungusungu kutoka tawi  la  Mwalukwa  wilaya ya Shinyanga  na  Selemani Kanoni  kutoka tawi la  Ikonongo wilaya ya Kishapu walisema kuwa  wanashindwa  kuwakamata  kutokana na sungusungu kukosa nguvu  ya kuwa na silaha ikiwa wanaohujumu uchumi huja na silaha hivyo wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha ili kukomesha wizi huo.
 

0 Response to "MASHIRIKA YA UMMA YAPATA HASARA KUBWA KUTOKANA NA KUIBIWA KWA MIUNDOMBINU YAKE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.