Habari za hivi Punde

MWENYEKITI CCM MKOANI SIMIYU ASISITIZA WANANCHI MUUNGANO WA SERIKALI MBILI



MWENYEKITI  wa chama cha Mapinduzi  (CCM)  mkoani Simiyu ambaye pia ni  mbunge wa jimbo la Busega dkt  Titus Kamani ameendelea kusisitiza muungano wa serikali mbili  kwa sababu waasisi wa wazamani wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Abed Karume walikaa na kujadili mafanikio ya muungano wa Tanzania na kusisitiza uwepo wa serikali mbili.

Mbunge huyo ambaye ni waziri wa maendeleo ya uvuvi na mifugo alisema  ni  busara za waasisi hao za kusistiza muungano na kuenzi zilizopelekea kuundwa kwa muundo wa serikali mbili zimesababisha hali ya muungano mpaka sasa kuwa imara na kuleta amani baina ya watanzania, na kutaka muundo huo ni vyema ukaendelea ili kulinda muungano.


Kamani alisema hayo  juzi katika mapokezi ya pikipiki ya umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi ccm kutoka Mkoani Mara na Mkoa wa Simiyu yenye lengo la kuwaunganisha vijana kuwa na ushirikiano na kuleta amani na utulivu  nchini.

Alisema wapo watu ambao kupitia katika siasa wanajaribu kuharibu muungano wa Tanzania kwa sababu tu wao wanamasilahi yao binafsi na vyama vyao wala sio kwa ajili ya kuleta maendeleo hapa nchini ili wananchi  waweze kujikwamua kimaendeleo.

 Alisema kuwa bunge la katiba kwa sasa limejikita katika kujadili mambo ya muungano lakini kwa vyama vyote vya upinzani  vinataka kuwepo na serikali tatu za Serikali ya Zanzibar,Tanganyika na ya Muungano kwa kutokutambua waasisi wa muungano huo walijadili kwa kina kuhusu muungano huo.

 “Kwa sasa  jicho la watanzania linatazama bunge lakini  unashangaza wabunge kutoka vyama vya upinzani wanapoingia bungeni kuanza kupinga, huku katika kamati zao wao huwa wanakubaliana”alisema  Kamani.

Alisema suala la serikali tatu linahitaji gharama kubwa katika kuendesha shughuli zake, sambamba na kuwepo kwa hali vurugu kama ilivyo katika mataifa ya sudani, Tuisia pamoja na Somalia chanzo kikubwa kikiwa ni mgawanyo wa mali.

 Hivyo aliwataka  wananchi kusoma kwanza  rasimu hiyo itakapofika kwa ajili ya kupigia kura pamoja na kuwa  makini kupiga kula wasije wakaamua kitu kikawa na madhara,wajumbe  wapige kura serikali mbili kutokana na kuizoea hivyo hakutajiki  marekebisho yeyote zaidi ya kuboresha muungano.


0 Response to "MWENYEKITI CCM MKOANI SIMIYU ASISITIZA WANANCHI MUUNGANO WA SERIKALI MBILI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.