Habari za hivi Punde

UMOJA WA VIJANA CCM (UVCCM) KANDA YA ZIWA WATAKA MUUNDO WA SERIKALI MBILI




UMOJA wa vijana  wa chama  cha Mapinduzi    kanda ya ziwa  (UVCCM) umewataka watanzania kutokubali muundo wa serikali tatu na kuwaeleza kuwa  iwapo zitakuwepo hizo serikali  upatikanaji wa  fedha zinazotokana na ulipaji kodi  hazitatosheleza ikiwa  jamii bado zinahitaji  huduma   bora   kwenye  afya,elimu na  mambo mengine .

 

  Hayo wameyasema kwenye matembezi ya mbio za pikipiki  ya muungano  taifa yaliyoandaliwa na umoja wa vijana  wa chama cha Mapinduzi (UVCCM)  taifa  ambapo matembezi hayo  yalikuwa yamebeba ujumbe wa  dumisha  muungano  vijana  kwa fursa  zilizopo kwa maendeleo yetu,  kwa mkoa wa shinyanga yalipokelewa kutoka mkoani Simiyu  katika kijiji cha Wigelekelo  wilayani Maswa.

 

Kiongozi wa matembezi ya mbio hizo  kanda ya ziwa Zuberi Bundala alisema kuwa  wameamua kuzunguka wilaya zote za kanda kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi  ikiwa baadhi ya vyama  wanadai kuwepo kwa serikali tatu  jambo ambalo litafanya jamii kukosa mambo ya msingi kwa kupitia kodi wanazolipa.

 

Akitoa ujumbe huo  katika mikutano  ya  hadhara kwa nyakati tofauti  kwa wananchi wa wilaya ya Kishapu na   Manispaa  ya Shinyanga Bundala  alisema  kuwa serikali mbili ndizo zinatoa fursa ya mwananchi kuona kodi yake inatumika vipi kuliko hiyo serikali tatu ambayo inapiganiwa na baadhi ya  vyama ,hivyo  wapiganie wao hizo serikali na kutoa hoja za msingi kwa wananchi .

 

 Alisema    kwa mujibu wa taarifa  ya maoni ya wananchi  kupitia rasmu ya katiba iliyowasilishwa  na  aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Joseph Warioba  kwenye bunge maalumu la katiba mjini Dodoma alisema   kuwa  asilimia 61 imependekeza  serikali  tatu hivyo vijana  watahakikisha wanapigana kutetea  maslahi ya wananchi kwa kutaka serikali mbili.

 

“Sisi kama vijana wa chama cha Mapinduzi tunataka serikali mbili ambazo wananchi wanalipa kodi na kuona matokeo ya kodi zao sasa ije hiyo serikali tatu kodi itaonekanaje?,  kama vyama vya upinzani wanataka serikali tatu waipiganie  na kutoa hoja za msingi , hivyo wajumbe ambao ni wabunge  wa bunge la katiba nao wanaonekana kushindwa basi warudi nyumbani na kurudisha pesa walizozitumia mpaka sasa,vijana tumeahidi kupigana na kutaka maslahi ya  wananchi yasipotee.”alisema.

 

Naye mwenyekiti wa umoja wa vijana  CCM mkoani  wa Shinyanga  Mapinduzi  Henry alisema  kuwa  muundo wa serikali mbili ndio unaofaa hivyo vijana wasikimbilie serikali tatu ambazo kwa kuangalia malengo  yake  baadaye ni kuwakandamiza wenye kipato cha chini ikiwa wanatumia kodi zao kupata maendeleo hiyo nyingine  ya tatu ni mzigo kwa wananchi.

 

Hata hivyo  mbunge Selemani Nchambi  kutoka jimbo la  Kishapu na  mbunge  Steven Masele kutoka jimbo la Shinyanga mjini walisimama kwenye  mikutano hiyo ya hadhara huku kila mmoja  katika jimbo lake akiwaeleza wananchi kukataa kwa  serikali tatu  na kueleza    faidi zinazopatikana kwenye muungano wa sasa  kuwa anayetoka Zanzibar anamiliki ardhi ya Tanzania bara bila  wasiwasi  huku kodi zikimnufaisha   mlipa kodi wa Tanzania bara.

 

  Katibu wa chama cha Mapinduzi    mkoa wa Shinyanga Adamu Ngalawa alisema  kuwa  suala la serikali tatu litaonyesha kuwatenga  baadhi ya raia ikiwa kunamzaliwa kutoka Tanzania bara na Zanzibar na mwingine  hayuko pande zote sula la kujiuliza watapewa uraia wa upande upi ?.

 

Ambapo mwenyekiti wa chama hicho  mkoa Khamis Mgeja alisema kuwa   baadhi ya watu wanaubeza muungano  huku wengine wakidai hati ya muungano,kazi  kubwa iliyopo sasa ni kutetea Tanzania na msimamo uwe wa serikali mbili ikiwa wakati wa uchaguzi mwaka 2010 sera zilizowasilishwa  za kila chama , lakini sera ya  CCM ilionyesha ni jinsi gani bado inahitaji serikali mbili na muungano bado haujapoteza uhalisia wake.

 

Hata hivyo matembezi hayo ya kuuenzi muungano wa miaka 50 wa  Tanzania bara  na  Zanzibar  ulinzinduliwa rasmi tarehe 22 march mwaka huu   na  rais wa Zanzibar  Dtk  Mohamed Shein huku kanda ya ziwa yalianza  rasmi tarehe 11 mwezi  huu mkoani Mara.

 

0 Response to "UMOJA WA VIJANA CCM (UVCCM) KANDA YA ZIWA WATAKA MUUNDO WA SERIKALI MBILI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.