Habari za hivi Punde

WAEKEZAJI MANISPAA YA SHINYANGA WALALAMIKIWA.



WAWEKEZAJI   manispaa ya Shinyanga wamelalamikiwa kutotekeleza  matakwa waliyokubaliana mara baada ya kuwa wameomba kuwekeza  maeneo mbalimbali na kuchukua ardhi kubwa jambo ambalo limefanya kuzua migogoro mikubwa kwenye maeneo  ya wakazi hao.

Kitu kilichobainika mara baada ya kukaa  kamati ya miundombinu ya madiwani,ilijionea  mwekezaji katika eneo la N’helegani alichukua ekari  zaidi ya 100 huku akiahidi kujenga  madarasa  kwaajili ya kuanzisha shule ya wakulima , kuajiri  wafanyakazi wazawa huku wawekezaji wengine wakiahidi pia kuweka  kiwanda cha kusindika nyama   mambo ambayo yamekwenda kinyume.

Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa kamati ya miundombinu  ambaye pia ni diwani wa kata ya Chamaguha  Morice  Mghin   kwenye  baraza la madiwani   lililofanyika  katika ukumbi wa mkoa huku akieleza kuwa  kutokana na makubaliano hakuna madarasa yaliyojenga wala shule, hakuna ajira iliyotolewa  matokeao yake  wananunua  marobota na kutenge nyuzi kwa kusafirisha nje ya nchi.

“Jambo lingine  wawekezaji  kampuni ya  wachina eneo la ibadakuli  tulikubaliana  kiwanda cha kusindika nyama  wanachokifanya wanasindika ngozi  pekee tena   wameajiri vijana  wanaowatumia  bila vitendea kazi mikono yao imeanza kuchumbuka  hivyo wanaonekana  kutotii sheria ya Osha,huku mwekezaji  kampuni ya jambo  akilalamikiwa kuchukua eneo zaidi tofauti na alivyopimiwa hali ambayo imezua migogoro  kwa wananchi wa eneo hilo  na kiasi cha zaidi ya shilingi  millioni 400 bado hakijalipwa.”alisema Mghini.

Hivyo alitoa ushauri kuwa  suala la wawekezaji  limeonyesha kuwa na ubabaishaji  kila wanapofuatwa hukumbilia  kwa mkuu wa mkoa  utaratibu uwepo  wa  wawekezaji  kupitia kwa wakurugenzi   wanaotoa ardhi   na uwe wa hisa  na sio uanzie mkoani kama ulivyo sasa  ambapo  imeonekana wananchi  kuwakosesha  haki zao za msingi.

Diwani wa kata ya Ibadakuli  Leonard   Richard  alisema kuwa kumekuwepo mgogoro wa ardhi  eneo hilo  kampuni ya jambo  kuchukua eneo zaidi  huku  Siri Yasin  diwani viti maalumu akieleza  kuwa   baadhi ya watumishi wamekuwa wakiegemea upande wa wawekezaji  bila kushirikisha  wananchi jambo ambalo linaonyesha kujidhalilisha  ikiwa wanatakiwa kuanzia uongozi wa vitongoji,vijiji na kata ambapo kunapatikana ukweli sio   kwenda   kwa mwekezaji.

Naye naibu  mstahiki meya  wa manispaa  David Nkulila alisema kuwa  hakuna sheria inayoua sheria   wawekezaji wamekuwa wakienda kinyume  na kuleta ubabaishaji  ikiwa wameonekana dhahiri pindi wanapofuatwa na  maafisa  mbalimbali hujifanya kutofahamu lugha  hasa hawa wachina  na mwisho wa siku humfuata mkuu wa mkoa na kutoa malalamiko yao.

Kaimu mkurugenzi  ambaye pia  ni ofisa ardhi wa manispaa  Dismas  Minja alisema kuwa yanayosemwa ni kweli   ila kinachotakiwa  ni kuanza  ufuatiliaji  wa karibu ili wananchi wanufaike  na ardhi yao, hivyo inatakiwa kuwa macho  na wawekezaji  wa namna hii haiwezekani wanachukua ekari 150 na hakuna kitu chochote kinacho fanyika  kwa wananchi.

Katibu  tawala wilaya.  ya Shinyanga  Boniface  Nchambi alisema kuwa   suala la mgogoro wa ardhi  limekuwa ni changamoto kubwa kwenye maeneo yaliyochukuliwa na wawekezaji  hivyo  uamuzi uliopo  waorosdheshwe   watu wote waliochukuliwa maeneo yao ili kuweza kubaini tatizo liko wapi.


0 Response to "WAEKEZAJI MANISPAA YA SHINYANGA WALALAMIKIWA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.