Habari za hivi Punde

WAZAZI WAHIMIZWA KUONA UMUHIMU WA CHANJO KWA WATOTO


WAZAZI  na walezi  wilayani Maswa mkoani Simiyu wamehimizwa kuona umuhimu wa chanjo kwa kuwapeleka watoto  kupata chanzo  mbalimbali  za kuzuia maradhi ya kuhara na Nimonia zinazostahili kupatiwa kwa watoto walio chini ya mwaka mmoja ikiwa zaidi ya watoto 13,000 hawakupatiwa chanjo.

Changamoto mbalimbali katika utekelezaji wa zoezi hilo ambazo ni pamoja na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu na ukamilishaji wa chanjo zote,watotohao  hawakupata au kukamilisha chanjo sabau  ikielezwa ni  ukosefu wa usafiri kwa ajili za kliniki za mkoba za chanjo kwa baadhi ya vituo vya
kutolewa huduma za afya.

Mganga Mkuu wa wilaya  hiyo Dkt  Jonathan Budenu alibainisha hayo katika uzinduzi  wa wiki ya chanjo  uliofanyika katika zahanati ya kijiji cha Malita kata ya Zanzui  na kuhudhuria  na baadhi ya wananchi  hasa akina mama wachache waliojitokeza

.

“kiwango cha ufanisi kwa chanjo ya Pentavalent 3 inayozuia magonjwa matano ambayo Kifaduro,Dondakoo,Pepopunda,Homa ya Ini na Homa yaUti wa mgongo kimeongezeka kutoka asilimia 82 mwaka 2012 hadi asilimia 93 mwaka 2013”alisema dtk Budenu.

Alisema  kwa  wilaya  hii kiwango cha ufanisi kwa chanjo ya
Pentavalent 3 kimeongezeka  ikiwa  mwaka 2012  hadi 2013 watoto  zaidi ya 18,000 walichanjwa kati  ya  watoto  19,807 .

Naye  mkuu  wa wilaya hiyo Luteni Mstaafu Abdalah Kihato Alisema  watoto  ni binadamu dhaifu  wanahitaji uangalizi wa karibu  hawana wanachokijua isipokuwa  kupata maziwa ya mama  ikiwa  chanjo zilizozinduliwa za  kuhara(Rotavirus)na Nimonia(PCV 13) kwa watoto wa chini ya mwaka  mmoja ni lazima kuzipata.

“Chanjo iliyokamilika ndiyo msingi wa kuwa na afya njema kwa mtoto na kuzuia maradhi  mbalimbali yanayosumbua watoto hivyo itakuwa vigumu kwa mtoto kupata maradhi kwa sababu mwili utakuwa na kinga ya maradhi kwa miaka mingi”alisema  Kihato.

Hata hivyo  aliwataka  wazazi kuwapeleka watoto wao kwenye vituo ili
kupatiwa chanjo hizo  iwapo watatozwa fedha  na muuguzi
yeyote  wakati wa chanjo hizo  ni kinyume cha utaratibu kwani  hupatikana bure bila gharama yoyote.


0 Response to "WAZAZI WAHIMIZWA KUONA UMUHIMU WA CHANJO KWA WATOTO"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.