Habari za hivi Punde

ZAHANATI YA KIJIJI CHA SINGITA KATA YA USANDA YAKABILIWA NA UHABA WA MAJI,MAABARA NA DAWA.



ZAHANATI ya kijiji cha  Singita kata ya Usanda wilaya ya Shinyanga inakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji hali ambayo inayowalazimu mama  wanaokwenda kujifungua  kununua maji dumu la lita  ishirini shilingi mia mbili ikiwemo ukosefu wa maabara.

Wakiongea na waandishi wa habari waliotembelea zahanati iliyopo kijijini hapo,walisema kuwa  wanapokwenda kujifungua  hulazimika kununua maji kwaajili ya kufulia nguo na kuoga jambo ambalo limekuwa ni changamoto  kwao yakuwafanya kutumia gharama kubwa  huku kipato chao ni kidogo.

Walisema kuwa Zahanati hiyo haina huduma ya maji hulazimika kununua dumu moja la lita ishirini shilingi miambili ambayo ndiyo changamoto kubwa  ikiwemo ukosefu  wa dawa mara kwa mara,maabara  na baadhiya ya vifaa tiba ikiwa hulazimika  kufuata vipimo vingine katika hospitali ya serikali ya  mkoa au binafsi zilizoko mjini.

“Katika suala la maji tunatumia gharama  kununua dumu moja  shilingi 200  kwa kipindi hiki cha masika lakini msimu wa kiangazi maji huwa adimu tunalazimika kununua dumu moja mpaka shilingi 600 ili kuweza kuoga na kufua pindi tunapojifungua,isitoshe kuna uhaba wa dawa, maabara ya kupata vipimo vya magonjwa mengine kama kifua kikuu,kichocho na mengineyo”alisema  mkazi wa kijiji hicho Hawa John.

Naye diwani wa kata  hiyo Abeid Aljabir alikiri kuwepo kwa uhaba wa maji katika Zahanati hiyo  ikiwa tayari kuna mambomba ambayo tangu yawekwe hayajawahi kutoa maji hivyo imekuwa ni changamoto kubwa katika jamii  kununua maji huku kipato chao ni kidogo aliiomba serikali kuwapatia maji kutoka mradi wa ziwa Victoria  ili kuondoa kero hiyo.

Kwa upande wake  muuguzi  wa zahanati  hiyo Leticia  Anthony alisema kuwa kweli Zahanati  inachangamoto ya uhaba wa maji hivyo hata wao hulazimika  kununua kwaajili ya matumizi ya usafi,pia akina mama hao wanapokuja kujifungua hulazimika kununua maji ya kuoga na kufulia dumu lenye lita ishirini shilingi 200.

“Kweli  zahanati hii haina maabara,vifaa tiba,vifaa vilivyopo ni kwaajili ya upimaji malaria na maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) ikiwa wastani wagonjwa  kwa siku ni 60 hadi 70 zaidi ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano huja kwa maradhi ya malaria na wakubwa kwa maradhi ya kikohozi ambapo wanaokwenda kujifungua kwa mwezi hufikia zaidi ya 40”alisema Antony.

Naye ofisa  afya kata ya  Usanda  Mussa Chande  alisema kuwa Zahanati hiyo inahudumia vijiji vitano vya  Singita, Shagaluba,Manyada, Nzagaluba, na Igaganulwa.  ikiwa  kwa  kata nzima  kuna idadi ya watu zaidi ya 15,000

0 Response to "ZAHANATI YA KIJIJI CHA SINGITA KATA YA USANDA YAKABILIWA NA UHABA WA MAJI,MAABARA NA DAWA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.