Habari za hivi Punde

BAADHI YA VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI WAKITOA MALALAMIKO YAO DHIDI YA MIFUKO YA HIFADHI.


Mwenyekiti  wa chama cha watumishi wa serikali za mitaa TALGHU tawi la Shinyanga  Christopher Malengo alipokuwa akiwasilisha malalamiko dhidhi ya mifuko ya hifadhi kuwa imejikita kusaidia wafanyakazi  na kutumia  fedha hizo kwaajili ya uwekezaji ,ikiwa alishauri kuwa  wenye mifuko hiyo watengeneze utaratibu wa kuwekeza kwa kukopa wafanyakazi  pindi bado wawapo kazini kuliko kusubiri uzeeni,
Hata hivyo aliwaeleza mamlaka ya mifuko ya hifadhi  SSRA  kuwa mwajiri anachangia asilimia 15,  mwajiriwa asilimia 5,na kuchukua baada ya miaka zaidi ya 20  sasa kwanini usiwepo utaratibu pia wa  hao wenye mifuko kuchangia nao asilimia mbili.


Baadhi ya  viongozi wa  vyama vya wafanyakazi wakiwa katika moja ya semina iliyoandaliwa na mamlaka ya mifuko ya jamii nchini  SSRA ,ambapo walieleza kuwa kwanini usiwepo mfuko mmoja wenye kuleta mlingano wa mafao kuliko hivi sasa kumekuwepo na ubabaishaji mwenye miaka michache kazini kulipwa zaidi kuliko aliyefanya miaka mingi,huku baadhi ya mifuko imekuwa haitoi  maelezo kwa wateja wao.


0 Response to "BAADHI YA VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI WAKITOA MALALAMIKO YAO DHIDI YA MIFUKO YA HIFADHI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.