Habari za hivi Punde

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI KATA YA TINDE KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA


Mbunge viti maalumu Azzah Hillai akimueleza naibu waziri wa maji Amosi Makala  uhaba wa maji safi na salama katika kata ya Tinde  ambapo waziri huyo alitembelea miundombinu mbalimbali ya maji ili kujionea hali halisi.
Ikiwa baadhi ya wananchi walimuletea maji wanayotumia kwa kunywa  kama hapo  yanavyoonekana meza kuu kwenye jagi na chupa.


Baadhi ya vijana wakiwa na mkokoteni  unaokokotwa na punda  utakao beba madumu ya maji kwa lengo la kuyapeleka mjini  na kufanya biashara ikiwa dumu moja ni shilingi 300 hadi 400.


Naibu waziri wa maji akionyesha  bwawa la jomu lililopo kata ya Tinde ambalo hutegemea maji yake kwa kunywa  na dumu moja huuza shilingi 200 kwa maji yanayotoka kwenye mto huo,huku diwani wa kata hiyo Jafari Kanoro akieleza kuwa maji hayo yamekuwa yakisaidia ila kinachotakiwa uongozi wa wizara na halmashauri ulione suala hilo la kusafisha magugu maji hayo ndiyo imekuwa kilio chao kikubwa.


Naibu waziri akiwa katika mkutano wa hadhara,baadhi ya wananchi walimpelekea maji ili naye anywe ikiwa alinyanyua chupa moja ya maji na kuwaonyesha kuwa anao uwezo wa kunywa maji hayo ila kinacho takiwa ni kupatikana kwa maji safi  na salama ya kunywa
Ambapo aliwaahidi   muda sio mrefu watapata maji hayo,huku akiwataka wataalamu kutoka wizarani kushughulikia suala hilo ndani ya siku 14  huku akiwataka wananchi pindi watakapo kuja kufanya utafiti wapewe ushirikiano na kusiwepo mgogoro wa aina yoyote hivyo wizara itahakikisha mashine ya kuchimba kisima kirefu inakuja Tinde na kazi inaanza mara moja.


0 Response to "ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI KATA YA TINDE KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.