Habari za hivi Punde

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA KUJENGWA KIJIJI CHA NEGEZI KATA YA MWAWAZA MANISPAA YA SHINYANGA.


wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM mkoa wa Shinyanga wakifutilia kwa ukaribu ujenzi unaoanza kwaajili ya hospitali ya rufaa ya mkoa  ambapo ziara hiyo iliongozwa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga
ambapo ujenzi huo unajengwa katika eneo la kijiji cha Negezi kata ya Mwawaza manispaa ya Shinyanga.


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Rufunga akiwa kwenye eneo linalojengwa hospitali ya rufaa ya mkoa  akimueleza mwenyekiti wa CCM mkoa Khamis Mgeja ambapo ujenzi huo utagharimu  kiasi cha shilingi  billioni  89.6.


Baadhi ya mafundi wakiwa kwenye eneo la ujenzi huo ambapo wameanza kuchimba msingi.


Wajumbe hao wakiangalia eneo hilo na jinsi ya ujenzi unavyokwenda ambapo inaelezwa kuwa  pindi itakapo kamilika hospitali hiyo itaweza kuondoa msongamano wa wagonjwa  katika hospitali ya mkoa  ikiwemo wagonjwa kusafirishwa au kusafiri umbali mrefu kwa lengo la kutafuta matibabu.


0 Response to "HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA KUJENGWA KIJIJI CHA NEGEZI KATA YA MWAWAZA MANISPAA YA SHINYANGA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.