Habari za hivi Punde

MAMLAKA YA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII YATAKIWA KUSIMAMI ILI KUONDOA UTAPELI UNAOFANYWA.

BAADHI ya wajiriwa  katika sekta mbalimbali mkoani Shinyanga  wameitaka  mamlaka ya mfuko wa hifadhi ya jamii nchini  (SSRA)  kuzisimamia hifadhi zilizopo ili kuacha kufanya kazi kwa kutapeli  bila kueleza  viwango vya fedha  wanavyokusanya hali ambayo imejidhihirishia hata kipindi cha kustaafu kupokea mafao yao kidogo tofauti na wanavyotarajia.

Hata hivyo imebainika kuwa watumishi wapya wa serikali hususani waajiriwa wapya kutoa fomu ambazo zimeshajazwa bila kutoa ushauri  mzuri, hali ambayo inasababisha baada ya muda wateja wao kujutia kujiunga na baadhi ya  mifuko hiyo.

 Changamoto hiyo ilitolewa na  mkuu wa wilaya ya Shinyanga Annarose Nyamubi kwenye semina ya elimu juu ya hifadhi ya jamii kwa viongozi wa  mkoa wa Shinyanga na halmashauri ,ambapo alisema baadhi ya mifuko haifanyi kazi zake kwa uwazi  hivyo kuwatapeli watumishi hasa waajiriwa wapya.

 “Mifuko hiyo  inatakiwa kufanya kazi zake kwa uwazi na kutoa huduma iliyobora kwa wateja wao ili kuwahamasha watumishi wengine kutoka serikalini,mashirika,taasisi na watu binafsi kujiunga ili kujiwekea akiba ya uzeeni pamoja na mafao mengine ukiwemo uzazi na matibabu”alisema Nyamubi .

Alisema kuwa kitendo cha  mtumishi kufanya kazi  kwa muda wa miaka 30 na kufanananishwa  na yule aliyefanya miaka mitano kinaumiza  ikiwa leo hii  gharama za maisha zinapanda kila kukicha kinachotakiwa  wasimamizi wa mifuko hii  kwenda na mabadiliko ya hali halisi iliyopo.

Nyamubi alisema mfuko wa hifadhi ya jamii(NSSF) umekuwa ukilalamikiwa na watumishi wengi kwa kushindwa kuboresha huduma zake, hali hiyo inaweza kusababisha kukosa wananchama na malengo yao kutofikiwa na kutolea mfano wakati wa mei mosi mabango mengi yalikuwa yakiulenga mfuko huo kwa kuumiza watumishi katika mafao.

Kwa upande wake mwezeshaji wa semina hiyo kutoka (SSRA) Dar es salaam ambaye ni afisa mipango na rasilimali watu  Mohamed Nyasama,alisema mpaka sasa ni  asilimia 4.5 ya watanzania wote ndiyo wamejiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii,idadi ambayo bado iko chini tofauti na ambao hawapo kwenye mfumo wa ajira rasmi.

Alisema mamlaka hiyo inafanya kazi ya kutetea na kulinda maslahi ya wanachama,wafanyakazi na wastaafu ili kuleta faida kwa wateja kwa kuboresha uhakika wa maisha yao ya baadaye,kinga dhidi ya majanga kwa watanzania na kukuza uwekezaji nchini.

Katibu tawala wilaya ya Shinyanga Boniphace Chambi alisema utendaji mbovu wa baadhi ya mifuko unakatisha tamaa  watumishi kujiunga na mifuko yao, kutokana na kuona hali halisi jinsi wazee wastaafu wanavyohangaika kufuatilia mafao yao wakati takwimu zote zipo lakini kwenye malipo inakuwa tatizo.
 
Naye  Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoa wa Shinyanga (TUCTA)Fue Mlindoko,alisema kero kubwa wanazokumbana nazo ni mafao kutokuwa sawa miongoni mwa watumishi wakati wakitambua tarehe za kuajiriwa na kustaafu kwao , lakini cha kusikitisha inaoneka  ofisi za hifadhi hizo haziweki kumbukumbu nzuri ndio maana huwaomba tena uthibutisho wa kazi  jambo ambalo limekuwa ni usumbufu.
.

0 Response to "MAMLAKA YA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII YATAKIWA KUSIMAMI ILI KUONDOA UTAPELI UNAOFANYWA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.