Habari za hivi Punde

ZAIDI YA WAKULIMA 14,000 WAMEBAINIKA KUPATA HASARA KWA KUTUMIA MBEGU ZISIZO NA MANYOYA NA KUTOOTA. VIZURI




IMEBAINIKA kuwa  wakulima wa zao la pamba  zaidi ya 14,000 nchini wamepata hasara baada ya kupanda ekari 50 elfu kwa kutumia  mbegu zisizo na manyoya za Quiton na kushindwa kuota, huku wilaya ya Kishapu ikiwa ni miongoni  kwa kupata hasara ya billion 1.6 ambazo zingetokana na kuuza zao hilo.

Katika mikoa sita na wilaya 23 ,ambapo ekari 50 ,000 hazikuota  zilizopandwa kwa kutumia mbegu ya quiton UK 91 na UK 08 ,ambazo zilifanyiwa utafiti katika chuo cha Ukiriguru jijini Mwanza na kuonekana zinafaa kwa kuwa na ubora mkubwa utakaosaidia kuongeza uzalishaji

Ufafanuzi wa tatizo la mbegu  hizo  kutoota kwa wakulima lilitolewa  wakati wa ziara ya Naibu waziri wa kilimo chakula na ushirika wilayani Kishapu ambapo  mkurugenzi wa huduma za usimamizi bodi ya pamba Tanzania James  Shimbe,alisema  katika mikoa inayolima pamba ni  Mara pekee ndiyo ambayo haikuathirika kutokana na mbegu bora ambazo wanazalisha wao .

“Tulifuatiliaili kuona  baadhi ya maeneo mbegu hizo  kwanini zishindwe kuota, lakini kulibainika  mambo  mbalimbali  ikiwa  baadhi ya mifuko ya mbegu ilikutwa na fangazi na kuwa na unyevunyevu na kubadilika kuwa nyeusi,wakulima hawakupata elimu ya kutosha jinsi ya kupanda na utunzaji pia mbegu hizo ”alisema Shimbe.

Hivyo bodi ya pamba  itahakikisha  inatafuta njia sahihi ya kumaliza tatizo hilo ili lisiweze kujirudia kwa mara nyingine, kutokana na kusababisha hasara kwa wakulima na baada ya kubaini hali hiyo tani 3117 za mbengu  zilisambazwa kwa wakulima ikiwa ni hatua ya kuwasaidia waweze kupanda tena.

Kwa upande wake Naibu waziri wa kilimo chakula na ushirika Godfrey  Zambi aliwatahadharisha viongozi wa serikali  kuwa makini na wanasiasa kutokana na baadhi yao kugeuza zao hilo kuwa sehemu ya siasa wakati wanaopiga kelele wakichunguzwa hawana hata shamba bali wababaishaji.

Alisema mbegu za quiton zimefanyiwa utafiti na chuo cha Ukiriguru na kubaini kuwa zinaubora  huku akisema tatizo liko katika usambazaji wa mbegu hizo,  jinsi ya kutunza  na upandaji kwani kampuni ya Quiton mkataba wake na wizara ni kuzalisha na siyo kusambaza.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Justine Sheka,alisema tatizo la  mbegu kutoota ni kubwa kwani katika wilaya hiyo wakulima zaidi ya 13OO mashamba yao hayakuota na hivyo kupata hasara ya zaidi ya billion 1.6.

0 Response to "ZAIDI YA WAKULIMA 14,000 WAMEBAINIKA KUPATA HASARA KWA KUTUMIA MBEGU ZISIZO NA MANYOYA NA KUTOOTA. VIZURI"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.