Habari za hivi Punde

MRADI WA BWAWA LA ISHOLOLO WAMSIKITISHA NAIBU WAZIRI WA CHAKULA KILIMO NA USHIRIKA ALIPOPATIWA MAELEZO JUU YA KUKWAMA KWAKE


MRADI  wa  mbwawa la umwagiliaji  katika kijiji cha Ishololo kata ya Usule halmashauri ya  wilaya  Shinyanga  umeingia  sura mpya mara baada ya naibu waziri  wa kilimo,chakula  na ushirika  Godfrey  Zambi  kuutembelea  na kujionea  hali halisi  ya kutokamilika  kwake ingawa  mkandarasi  ameongezewa muda  huku akisikitishwa na  uongozi ngazi ya kanda,mkoa  na wilaya kutoshirikishwa na kuutambua.

“Nina kiri  baadhi ya miradi  imetumia fedha nyingi zaidi ya shilingi  million 200 lakini miradi hiyo imefanywa vibaya ,pia serikali  ilidhamiria  kuweka mradi huu hapa  hali imeonekana mkandarasi  ndio hovyo na kutokuwa na uwazi  kwenye mradi,  ikiwa uongozi wa ngazi mbalimbali unaotegemewa haujashirikishwa.”alisema Zambi.



Ambapo  waziri huyo  mara baada ya kujionea alipewa maelezo na injia  wa skimu ya umwagiliaji Godrey Mbwambo kuwa  mkataba  wa mradi huo ulifungwa tarehe 15/02/2013 kati ya katibu mkuu na wizara ya kilimo chakula  na ushirika  na mkandarasi aitwaye SYSCON BUILDERS wa jijini Dar-es-salaam  chini ya mhandisi mshauri CODA AND PARTERS  ya Kenya  baada ya kufunga mkataba mkandarasi alitakiwa kuanza kazi mwezi mmoja  baada ya kufunga mkataba huo.

Mbwambo alisema  kuwa mradi huo  ulilenga kuwanufaisha  wakulima  na wafugaji  kutoka vijiji viwili vya Ishololo na Tindeng’hulu ambao ungeweza kunufaisha  wakulima  zaidi ya 1500 na kiasi cha hekta  zipatazo 500 zingeweza kumgwagiliwa  na maji kutoka katika bwawa hilo.

“Mradi huu ambao unafadhiliwa  na mradi wa uwekezaji katika sekta  ya kilimo wilaya (DASIP) imechangia kiasi cha  zaidi ya shilingi millioni  740 na mfuko wa umwagiliaji (DIDF) kwenye mradi huo imechangia kiasi cha shilingi  millioni 200 na kufanya jumla ya gharama  ya mradi  ya shilingi millioni 940”alisema  Mbwambo.

Pamoja na maelezo hayo  naibu waziri huyo alitaka  kupata majibu kutoka  ofisi ya kanda ambao walidaiwa kuwa  wahusika wa mradi huu,pia alisema  kushindwa kutekelezeka  fedha hiyo ninavyofahamu  itarudi benki ya Afrika  (AFDB) kwa kuwa mradi wa DASIP  uliisha muda wake 31/12/2013, ingawa inaelezwa aliongezewa muda na kushindwa kukamilisha pia.

Zambi alisema kuwa kweli  katibu  wa wizara ndio aliyesaini mikataba yote  hivyo yatahitajika  mazungumzo ofisini,,ikiwa mhandisi wa umwagiliaji kutoka ofisi ya kanda ya ziwa iliyopo jijini Mwanza Ebeneza Kombe alisema kuwa  mradi huo uliandikiwa  jumla ya shilingi billion 1.2 katika bajeti yake  ya mwaka 2013  lakini hazikuja  katika ofisi hizo  ililazimu  tena kuandika maandiko  mengine kwa kuanza upya.

Hata hivyo mbunge viti maalum Azzah Hilali  alimueleza  naibu waziri kuwa  ofisi  ya kanda wanyooshe maelezo  mradi huo wao  kama halmashauri na mkoa walielezwa hawahusiki bali ni ofisi ya kanda na wizara ikiwa wakulima  wamekuwa wakilalamika kushindwa kutekelezeka kwa wakati huku mkandarasi hana vifaa matokeao yake kufanya shughuli zake binafsi vijijini hapo.


Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Mohamed Kiyungi alisema kuwa  kiasi cha shilingi millioni  200 zilizotoka DIDF  na kuhamishiwa akaunti ya mradi wa DASIP Mwanza  wao kama halmashauri walikuwa wanaomba  fedha hizo zirudishwe kwenye akaunti ya halmashauri ili ziweze kuendeleza shughuli za miradi ya umwagiliaji.

Diwani wa kata hiyo Amina Bundala alisema kuwa alitakiwa kuanza  kazi tarehe 15/03/2013 na kazi hii ilitakiwa ifanyike ndani ya siku 240 sawa na miezi  nane ,licha ya kuongezewa muda  sisi viongozi tumeonekana waongo  sababu tangu mwezi huo mifugo  inakunywa matope badala ya maji  wakulima wamevurugiwa mashamba yao ikiwa  bwawa hilo linahitaji kuhudumia kata  za Bukene,Imesela  Usule na Tindenhulu.

Mradi huu uliibuliwa na wananchi wenyewe katika bajeti ya kijiji  ya mwaka 2011/12  kwa kutaka bwawa kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji  kwa zao la mpunga  ikiwa walikuwa wakikosa maji ya kutosha kwa kuliendeleza zao hilo  na kupata mavuno ya kutosha huku halmashauri ikipata pato la ndani  zaidi kupitia  ushuru za zao la mpunga.

0 Response to "MRADI WA BWAWA LA ISHOLOLO WAMSIKITISHA NAIBU WAZIRI WA CHAKULA KILIMO NA USHIRIKA ALIPOPATIWA MAELEZO JUU YA KUKWAMA KWAKE"

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.