Habari za hivi Punde

WAJASILIAMALI MANISPAA YA SHINYANGA WAPATIWA ELIMU YA KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI.

WAJASILIAMALI  manispaa ya Shinyanga  wamepatiwa elimu  juu ya kujiunga na mfuko wa hifadhi ya jamii ili kuweza kuboresha maisha yao na kuondoa dhana ya  mifuko hiyo  kuwa inawahusu waliopo kwenye sekta rasmi pekee kama ilivyo kuwa awali.

 Kwa sasa  mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa sekta ya mifuko ya hifadhi ya jamii (SSRA) imeamua kutoa fursa hata kwa wajasiliamali  wanaofanya biashara ndogondogo kujiunga na mifuko hiyo   kwa mujibu wa Hifadhi ya mifuko ya jamii ni haki ya kila mtu kujiunga nayo, haki hii imeanishwa katika ibara  ya 11 (1) ya katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na sera ya taifa ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2003.

Akitoa elimu   kwa wajasiliamali hao mwanasheria mwandamizi wa mamlaka hiyo Salma Maghimbi kutoka makao makuu Jijini Dar es slaam alisema moja ya wajibu wa mamlaka hiyo ni kutoa elimu kwa watanzania wote walioajiriwa na kujiajiri wenyewe ilikupanua wigo kwa wananchi kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii.

Maghimbi alisema mamlaka hiyo imeruhusu uandikishaji wa wanachama kutoka  sekta isiyo rasimi kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii mbalimbali hapa nchini ambao ni wakulima,na wafanyabishara ndogondogo (Wajasiliamali) kwa lengo la kupanua wigo mpana wa hifadhi ya jamii ulioendelevu na wenye huduma bora kwa kila mtanzania.

 “ Changamoto ya  sekta ya hifadhi ya  jamii  iliopo  inaonyesha takwimu  kuwa wananchi waliokatika sekta  rasmi wanaokadiliwa kufikia milioni  1.5 ndio wananufaika na sekta ya hifadhi ya jamii na watanzania waliowengi ambao wapo katika sekta isiyo Rasmi wamekuwa hawanufaiki na mifuko hiyo na kuwafanya kuwa na maisha magumu hasa pale wanapostaafu”.

Maghimbi alitaja faida zinazo patikana katika mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii kuwa ni mafao ya uzeeni, ulemavu, kuumia kazini, pamoja na kupata mikopo ya kuendeshea biashara na kukuza mitaji yao hali ambayo itakuza uchumi wanchi na kuongeza pato la taifa.

Akizungumza katika utoaji wa elimu kwa wajasiliamali hao ofisa Biashara wa manispaa ya shinyanga Erasto Mabina alitumia fursa hiyo kuwataka wafanyabiashara wa manispaa hiyo kujenga tabia ya kukata leseni za biashara ili kufanya biashara zao kiuhalali na kuchangia pato la serikali, fedha ambazo zitasaidia  kuendesha miradi ya maendeleo.
 
 kwa upande wa wajasiliamali hao kwa nyakatitofauti waliiomba mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii hapa nchini kuboresha huduma zao kwa wananchama na kuacha ubabaishaji na usumbufu ambao umekuwa ukilalamikiwa na baadhi ya wanachama waliojiunga na mifuko hiyo.

Baadhi ya  wajasiliamali wenzao Restuta Joseph na Ester Paulo waliishukuru Mamlaka hiyo ya usimamizi na udhibiti wa sekta ya mifuko ya  hifadhi ya jamii (SSRA ) kuwapa elimu na uelewa juu ya umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii hivyo watatumia vyema elimu hiyo kujiunga.
 

0 Response to "WAJASILIAMALI MANISPAA YA SHINYANGA WAPATIWA ELIMU YA KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.