Habari za hivi Punde

BAADHI YA MANENO WALIYOKUWA WAKITAMKA NA KUTAKA KURUDI CHADEMA.

hapo waliojivua chadema wakisubiri kupanda jukwaani ambapo aliyevaa shati la kijani  kuanzia kulia ni aliyekuwa diwani wa kata ya Maskelo anayefuatia ni diwani Sebastiani Peter wa kata ya Ngokolo manispaa ya Shinyanga.



Mbunge wa jimbo la Maswa Magharibi  mkoani Simiyu Slyvester Kasulumbai akituliza fujo iliyokuwa ikianz kutokea katika mkutano wa hadhara.


Kasulumbayi akiwapa maelekeza madiwani ambao walikuwa wamejiuzuru  ambao walikuwa juu ya jukwaa tayari kwa kuongea.

BAADHI YA MAELEZO WALIYOKUWA WAKIYASEMA JUKWAANI

WALIOJIVUA  udiwani  na uanachama  kwa tiketi ya chadema manispaa ya Shinyanga ambao ni Sebastian Peter  kutoka kata ya Ngokolo na  Zacharia Mfuko kata ya Masekelo kipindi hicho wakijiunga na  (CCM) wameibuka kwenye mkutano wa hadhara wa chadema   lengo lao ni  kuwapigia magoti kutaka kurudi ndani ya chama hicho tena.

Umati wa wananchi waliofurika  kujionea kwa mshangao waliokuwa wakiusikia na mwisho   kujionea  watu hao wakipanda jukwaani   ambapo walivua pia  sare za CCM  na kuvaa za chadema, kwa nyakati tofauti  walieleza kuwa walitekwa na kushawishiwa  mambo mbalimbali  yakiwemo kupatiwa fedha ili kukisaliti chama hicho.

Mkutano huo wa hadhara uliofanyika  katika viwanja vya  mahakama nguzonane  manispaa ya Shinyanga  ambapo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali   wa chama hicho kutoka kanda ya ziwa akiwemo mbunge wa jimbo la maswa  mashariki  mkoa wa simiyu Slyvester  Kasulumbayi Pamoja na  katibu mwenezi  wa kanda  ya ziwa  mashariki Joshua  Karando.

“Wanachama wenzetu tunaomba mtusamehe  kwani mambo haya yalitutokea kwa kushawishiwa na viongozi ndani ya CCM kuwa tukisaliti chadema leo hii tumekuja mbele zenu tunajutia maamuzi isitoshe hata kadi  za  CCM  hatukuchukua  tumerudi kundini  tunaomba mtusamehe  tuwe pamoja kama zamani “alisema diwani Sebastian.

Aidha  baadhi ya wafuasi wa chama hicho walionyesha hasira na kuanza kutaka kuleta vurugu ambapo mbunge  Kasulumbayi aliwatuliza huku akiwataka kusikiliza yale watakayoyaeleza ili kuona unyama unaofanywa na chama cha mapinduzi  kutaka kukivuruga chadema ili waendelee kushikilia dola,hivyo ujanja wao umebainika na hawa hawana makosa hakuna budi kuwasikiliza na kusamehe.
Pia  Kasulumbayi aliueleza umati huo  kuwa suala la kujiuzuru udiwani lilitendeka kimakosa kwani hata hizo barua hawakuandika wao bali waliandikiwa tena bila kufuata utaratibu kanuni na sheria kutoka mahakamani ikiwemo vielelezo vyote vya uchaguzi  wa ushindi walioupata  viwasilishwe ,kwahiyo inaonekana barua hizo  ni batili.

“Hawa wanahaki zote wametubu wanachadema wenzangu  ninaomba tuwapokee walifanya hivyo kimakosa,tusiwe na hasira  kwani kitendo cha kujiuzuru kinatakiwa kipite mahakamani kwenda kuapa sanjari na vielelezo vyote vinavyotakiwa hivyo  bado wanahesabika ni madiwani kwasababu hawakupitia taratibu kanuni na sheria katika kujizuru kwao”alisema Kasulumbayi.


0 Response to "BAADHI YA MANENO WALIYOKUWA WAKITAMKA NA KUTAKA KURUDI CHADEMA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.