Habari za hivi Punde

HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU IMEWEKA MIKAKATI YA KUNYANYUA ELIMU.


HII NI SHULE YA MSINGI MASAGALA ILIYOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU   NI KATI YA SHULE KUMI BORA ZILIZOFANYA VIZURI WILAYANI HUMO.

HALMASHAURI  ya wilaya   Kishapu mkoani Shinyanga  imeweka mikakati ya  kuboresha elimu ya shule  za msingi kwa kuziondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo  kukarabati maboma ya vyumba vya madarasa, kuongeza ufaulu kwa wanafunzi  wa darasa la saba  huku shule ya kwanza  ikizawadiwa  shilingi laki tatu na inayoshika mkia hupewa kinyago.
Hata  hivyo kimkoa katika ufaulu wa shule za msingi  ni asilimia 84 kwa upande wa  darasa la saba  mwaka jana kwenye   halmashauri hiyo  ikiwa   imeshika nafasi ya pili, pia kuna  shule za  msingi 114  tayari   wamepokea walimu 142 kwa mwaka huu   ambapo mahitaji ya walimu   wa shule za  msingi wilaya nzima  ni 1639.
 Hayo yalisemwa kwenye baraza la madiwani  la halmashauri hiyo  hivi karibuni  huku baadhi ya madiwani wakielezea changamoto ya elimu shule za msingi kuwa  uhaba wa madawati ,maboma mengi yamejengwa bila kukukamilishwa  ukiwepo udangangayifu kwenye mitihani  pia waelekeze katika shule kumi zilizofanya vibaya chanzo chake ni nini hasa.
Diwani wa kata ya  Sekebugoro  Fernand  Mpogomi  alisema kuwa  maboma yamekuwepo mengi  yameshindwa kukamilishwa walimu wana upungufu wa nyumba, uhaba wa madawati  sasa ni suala la kuelekeza kwenye elimu zaidi  na kutekeleza hayo mfano shule ya msingi Mwigumbi imeingia kwenye shule kumi ambazo zimefanya vibaya  nini tatizo ikiwa ina walimu wa kutosha na wanapata chakula cha mchana.
Diwani wa kata ya  Bubiki  Boniface Mataba alisema kuwa tatizo lingine kumekuwepo na michango  mingi masuleni  ambayo haina tija,wanafunzi wanapotoa fedha hawapewi stakabadhi   wakati mwingi hupewa lakini hazionyeshi ni mchango kwaajili ya nini,kama ni suala la maji ,mlinzi au ada basi ziandikwe na kuonekana  kwa kutofanya hivyo wazazi wanaona huo ni utapeli.
“Michango mashuleni ni mingi haina tija kwani hatuoni inafanya kazi gani,hata wakitoa wanafunzi hawapewi stakabadhi za malipo wakati mwingine haziandikwi kuwa ni malipo ya ada au kitu gani, sio kwamba  tunaikataa michango ila ionyeshe  imefanya shughuli  gani ndani ya shule husika”alisema diwani  Mataba.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Justine Sheka alisema kuwa  changamoto zilizopo zifanyiwe kazi kwa kuboresha miundombinu katika shule hasa kwenye maeneo yanayoelezwa kuwa ni tatizo,ikiwa kiasi cha shilingi  laki tatu hutolewa kwa shule inayofanya vizuri  na kinyango kwa shule  inayokuwa ya mwisho.
Ofisa elimu wa shule za msingi  katika halmashauri hiyo  Sostenece  Mbwilo  alisema kuwa kimkoa wilaya hiyo kwenye ufaulu  imekuwa  nafasi ya pili kwa kupata asilimia 84,ikiwa changamoto  ilionekana katika usimamizi  wa mitihani ya moko kuwepo udanganyifu tofauti  mitihani wa taifa  unavyokuwa makini  katika usimamizi wake.
Sostenece alisema kuwa  pia kumekuwepo na shule kumi bora ambazo zimefanya vizuri  ikiwemo shule ya msingi Mwadui  A na  Masagala ambapo alizielezea kuwa hazina changamoto kama shule zingine  za uhaba wa madawati, walimu wa kutosha walioendana uwiano na wanafunzi ukiwemo ukaguzi wa mara kwa mara  na utolewaji wa motisha kwa walimu wa masomo yaliyofanya vizuri.
Pia shule zilizofanya vibaya  zimelezwa kuwa na changamoto  ya mrundikano wa wanafunzi usioendana na  uwiano wa walimu, uhaba wa madawati , nyumba za walimu  ikiwemo ofisi ambapo  masuala hayo yote yanachangia   kushuka kwa elimu  hata ufaulu kwa wanafunzi hao.



0 Response to "HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU IMEWEKA MIKAKATI YA KUNYANYUA ELIMU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.