Habari za hivi Punde

USAWA KWENYE ELIMU KWA WATOTO WA KIKE BADO WILAYANI KISHAPU MKOANI SHINYANGA.

Mwezeshaji kutoka mtandao wa jinsia Tanzania Kenny Ngomuo akiwa katika semina ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga march mwaka huu,ambapo alieleza suala la utekelezaji wa masuala mbalimbali ikiwemo elimu,.

Hata hivyo bado asilimia 14 ya wanafunzi  wa  kidato cha kwanza kwa mwaka huu  wilayani Kishapu mkoani Shinyanga hawajaripoti shule  ikiwa idadi kubwa ni wasichana  huku ikielezwa  hakuna sababu yoyote iliyowafanya wasiripoti ambapo tayari wazazi wanne walifikishwa mahakamani  na kutozwa faini.


Hayo yalisemwa na  ofisa elimu vifaa na takwimu kwa niaba ya ofisa elimu wa sekondari  wa halmashauri hiyo  Paul  Kasanda  wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake  ambapo alisema kuwa  asilimia hiyo ni sawa na wanafunzi 190  zaidi wasichana  ambao hawajaripoti kwa mwaka huu mpaka sasa.

Alisema kufikia asilimia 14  ni jitihada zilizofanywa na watendaji wa vijiji na kata  kwani  kufikia mwezi march  mwaka huu kulikuwa na wanafunzi 525 ambao hawajaripoti  sawa na asilimia 22,lakini wazazi walikuwa wakifuatwa  wa watendaji hao  huku wakishindwa kutoa maelezo ya kwanini  hawawapeleki watoto wao shule.

“Hizo zote ni jitihada za watendaji wa vijiji na kata na kufikia asilimia 14, wazazi katika halmashauri hii hawana mwamko wa kuwasomesha watoto wao hasa wa kike hata idadi kubwa ya  watoto ambao hawajaripoti  kuanza kidato cha kwanza  ni wasichana  ndio maana hata suala la elimu linazidi kushuka  kwa upande wao ”alisema  Ofisa elimu.

Hata hivyo alisema kuwa  kwa mwaka huu, waliojiunga na kidato cha kwanza  jumla ni 2141 ikiwa wavulana ni  1222 na wasichana  919 ikiwa changamoto kubwa ni  kuripoti kwa wanafunzi hao mashuleni na wazazi kutokutoa ushirikiano wa kutosha.

Alisema kuwa Kati ya shule 25 za kata ,shule ya  sekondari  Somagedi  iliyopo kwenye kata hiyo imeshika nafasi ya kwanza  kiwilaya  huku kimkoa ikishika nafasi ya  tano ambapo wanafunzi waliofanya vizuri  kumi bora kiwilaya wasichana ni wawili pekee,wakati huohuo  mpaka sasa  wanafunzi wa kidato cha tano walioripoti ni  55  kati ya wanafunzi 83 waliochaguliwa kujiunga na  michepuo ya  HGK na HGE.

Aidha alisema kuwa  katika  michepuo  ya HGK wanafunzi waliochaguliwa ni  40 na HGE  ni  wanafunzi 43 ,Pia kuna walimu 365 na nyumba za walimu 85 ikiwa bado kunachangamoto ya ukosefu wa  shule za sekondari kwa kidato cha tano na sita  kwa wilaya nzima ipo shule moja .

Kwa upande wake diwani wa kata ya Mondo  John  Ndama alisema kuwa  watoto wa kike wanapaswa kuelimishwa  zaidi  ikiwa wanauwezo hata wa kuongoza  kiwila na kimkoa  kwa masomo yote kinachotakiwa ni uhamasishaji wa wazazi  kuwasomesha watoto wa kike kwa bidii na sio kuwabagua  na kuwadhoofisha kielimu.

0 Response to "USAWA KWENYE ELIMU KWA WATOTO WA KIKE BADO WILAYANI KISHAPU MKOANI SHINYANGA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.