Habari za hivi Punde

DIWANI WA KATA YA PONGWE MUHEZA AMECHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI.

HILI NI BARAZA LA MADIWANI MUHEZA.
 
BARAZA la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Muheza mkoani Tanga wamemchangua Rashidi Mdachi ambaye ni diwani wa kata ya Pongwe kuwa makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Katika uchaguzi huo uliofanyika juzi kwenye mkutano wa baraza la madiwani lililo la kawaida,Mdachi ameshinda kiti hicho baada ya kuchaguliwa kwa kupata kura 37 kati ya 40 zilizopigwa ambapo kura tatu zilimkataa.


Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Muheza,Amiri Kiroboto akimtangaza,Mdachi juu ya kushinda kiti hicho huku alisema kura zilizopigwa ni za ndiyo na hapana baada ya mjumbe huyo kupitishwa katika uchaguzi wa ndani wa CCM huku baraza likikosa wajumbe kutoka upinzani.

"Ndugu wajumbe sasa natakata kutangaza matokeo baada ya kufanikisha zoezi letu la kupiga kura,awali tulikubaliana kuwa kura zitakazopigwa ni zile za ndiyo na hapana ambapo sasa natangaza matokeo,Mdachi amepata kura 37 kati ya 40 na tatuz zimesema hapana"alisema.

Akitoa shukrani mara baada ya kutangazwa kuwa msindi Mdachi aliahidi kuendelea kutekeleza wajibu wake kwa ufanisi kama alivyokuwa akiwajibika awali katika nafasi hiyo ambapo pia aliwaomba wajumbe wenzake kuendelea kumpatia ushirikiano wa hali na mali.

Alisema kuwa ni lazima ieleweke kwamba hata yeye ni binadamu hivyo anahitaji kuelezwa pale anapokwenda tofauti ambapo itaweza kuwa vigumu kama hatakumbushwa ama kuelezwa juu ya pale ambapo amekwenda tofauti ili kuweza kujirekebisha ili kuweza kuwajibika kikamilifu.

Mdachi aliendelea kusema kwamba kitu kikubwa kinachohitajika kwa sasa ni juu ya kuongezeka kwa mshikamano miongoni mwa wajumbe na hata watendaji wa halmashauri njia ambayo itawawezesa kuwatumikia vyema wakazi wa halmashauri ya Muheza na vitongoji vyake.

Aidha makamu mwenyekiti huyo wa halmashauri ya wilaya ya Muheza alisisitiza kwamba atahakikisha kwamba utoro wa wanafunzi shuleni unadhibitiwa kwa kushirikiana na wadau wengine ambapo kwa kufanya hivyo sekta ya elimu itaweza kuimarika  na kuleta tija.

0 Response to "DIWANI WA KATA YA PONGWE MUHEZA AMECHAGULIWA KUWA MAKAMU MWENYEKITI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.