Habari za hivi Punde

USAFIRI HUU NI BURE KWA WAGONJWA WENYE KUHITAJI RUFAA,ASEMA MBUNGE.

BAADHI  ya   wananchi wa kijiji cha Igalamya kata  ya Usule  katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  wamelalamika kutozwa gharama ya shilingi 40,000 hadi 60,000  ya usafiri wa gari la wagonjwa (Abulance)pindi wanapokuwa na wagonjwa wanaohitajika  kwenda  kupata matibabu zaidi kwenye hopitali ya  rufaa ya mkoa

Hali hiyo imewafanya baadhi ya wagonjwa  kupoteza maisha wakiwa njiani huku  mama wajawazito kuzalia  majumbani au njiani kwa kukosa gharama hiyo ambayo ilikuwa ikitozwa na waganga wa  vituo vya afya  kwa kudai  ni gharama za mafuta ya kumpeleka mgonjwa hospitali ya rufaa  ambayo iko mjini.

Wananchi hao wakiongea kwenye mkutano wa hadhara  mbele ya mbunge wa jimbo hilo la Solwa  Ahamed Salum uliofanyika katika kijiji hicho,  mara baada ya  kukabidhiwa gari hilo baada ya kuharibika kwa muda mrefu bila kupatikana mtu wa kulitengenezai ndipo aliamua  mbunge kulitengeneza kwa gharama yake ya  shilingi millioni  7.5.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo  akiwemo Mariamu  Malale  na Elius  Bukwiba walisema kuwa  walikuwa wakitozwa kiasi cha shilingi  40,000 hadi 60,000  na uongozi  wa zahanati hiyo kwa kukodi  gari la wagonjwa  kumpeleka mgonjwa katika hopitali ya rufaa mjini hata ukiwa na mama mjazito wengi walikuwa wakitoa ambao hawana mara nyingi wagonjwa walikuwa wakizidiwa njiani  na kupoteza maisha.

“Mimi mwenyewe nimekwisha toa kiasi cha shilingi 40,000  kwaajili ya gari kumpeleka mtoto wangu hospitali ya rufaa mjini  ili kuweza kupata matibabu,nilipokuwa natoa pesa hizo nilielezwa kuwa ni gharama za mafuta kwasababu nilikuwa nataka mtoto wangu apone nilitoa sikufahamu kuwa ni bure kama inavyoelezwa sasa na mbunge kweli tumeteseka  na huo ndio utakuwa ni mkombozi wetu”alisema   Bukwiba.

Naye mbunge  wa jimbo hilo   Salum  alisema kuwa gari  hilo amelileta kwa matumizi  ya rufaa pekee ambapo watakuwa wakisafirishwa bure  atakaye toa pesa awe amependa mwenyewe, mafuta yatakuwepo kila wakati, ila wagonjwa watakao hitajika zaidi ni mama wajawazito  walioshindwa kujifungua, waliopata ajali na wagonjwa mahututi.

“Nataka niwaeleze kuwa  leo nimekuja kukabidhi gari lililowashinda kulitengeneza  sasa nimetengeneza kwa gaharama yangu ya shilingi millioni 7.5, litabeba wagonjwa waliomahututi bure  mafuta yatakuwepo kila wakati ila ninachowaomba  hii zahanati  malengo yake ilitakiwa kiwe   kituo cha afya kwani nilikwisha leta mifuko ya  saruji 262  haijulikani imekwenda wapi  nitaomba kamati iliyoundwa ya usimamizi wa ujenzi huo  inipatie maelezo”alisema Mbunge  Salumu.

Pia mkurugenzi wa halmashauri hiyo  Mohamed  Kiyungi alisema kuwa  huduma ya gari la wagonjwa ni bure hakuna wakuwatoza fedha ya aina yoyote  huku akiwahakikishia upatikanaji wa mafuta kwenye gari hilo utakuwepo hivyo wananchi wasiwe na hofu  juu ya hilo kinachotakiwa ni utaratibu wa utumiaji wa gari la wagonjwa sio kiholela.

Aidha alisema kuwa  wananchi wajitahidi katika mchango ili kuweza kufanikisha ujenzi wa  kituo cha afya ikiwa mbunge tayari kajitolewa mifuko ya  saruji hivyo  waweke umoja wa kujitolea hata ubebaji wa  michanga na kokoto kwenye ujenzi huo ili iweze kufanya kazi mara moja na kupunguza  matatizo ya kusafiri umbali mrefu.

0 Response to "USAFIRI HUU NI BURE KWA WAGONJWA WENYE KUHITAJI RUFAA,ASEMA MBUNGE."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.