Habari za hivi Punde

SHULE INAKABILIWA NA UKOSEFU WA CHOO CHA WANAFUNZI ZAIDI YA 500,PAMOJA NA WALIMU IKIWEMO MADAWATI.


HIKI NI CHOO KINACHOTUMIWA NA WANAFUNZI ZAIDI YA 500 SHULE YA MSINGI MAWEMILU.

SHULE ya msingi  Mawemilu iliyopo katika kijiji hicho kata ya Mwakitolyo  halmashauri ya Shinyanga inakabiliwa na  changamoto ya ukosefu wa matundu ya  vyoo vya wanafunzi pamoja na walimu hali ambayo inawafanya  kuwepo kwa uchafuzi wa mazingira kwa kujisaidia porini huku walimu wakitumia  vyoo vya familiza za walimu zilizopo karibu na shule hiyo.

Shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi zaidi ya 500 ikiwa wavulana 211 na  wasichana 300 ambapo  choo kilichopo kina matundu mawili   pekee hata miundombinu yake ni mibovu iliyojengelewa kwa  nyasi  huku walimu wakiwa 11 wakiume saba na wakike wanne,sanjari na  robo tatu ya shule  hukalia magogo ya miti wawapo darasani.
Mwandishi wa habari mara baada ya kujionea changamoto hiyo alifanikiwa kuonana na Mwalimu mkuu wa shule hiyo  Joseph Chagaka ambaye alikiri kuwepo kwa  changamoto hizo  huku akisema kuwa  awali kulikuwepo na  matundu ya vyoo sita kwa wanafunzi lakini yalititia  kutokana na mvua za masika zilizokuwa zikinyesha,kwa upande wa vyoo vya walimu  havikuwepo.
“Kweli changamoto hiyo  ipo sisi tuliamua kujenga choo hicho chenye matundu mawili na kujengelea kwa nyasi  wanafunzi watumie kwa  muda tukiwa tunaendelea kujipanga na ujenzi,nina amini havitoshelezi kwani kuna wanafunzi zaidi ya 500, madawati yapo 50 tu, walimu wapo 11 nyumba za walimu zipo mbili  ila choo cha walimu shuleni hapa hakuna hutumia vyoo vya kwenye familia za walimu.”alisema  mwalimu mkuu huyo.
Hata hivyo mwalimu mkuu huyo alisema kuwa kuna mahitaji  makubwa ya  madawati,matundu ya vyoo kumi na moja, vyumba vya madarasa ,walimu 21 na nyumba za walimu 11 ili kuweza kutosheleza,ila mikakati iliyopo ni kuzipunguza changamoto hizo zimekuwa ni kero hali ambayo imeonekana hata wanafunzi na walimu wenyewe kupata usumbufu . 
Naye  ofisa mtendaji wa kijiji hicho  Ezekiel  Deusi alisema kuwa  changamoto kubwa shuleni hapo ni vyoo  vilivyopo miundombinu yake ni mibovu ni sawa na hakuna vyoo kwani vilititia kipindi cha mvua  za masika na sasa mahitaji ni  matundu ya vyoo  11 ili kuweza kuondoa changamoto hiyo, mikakati ya ujenzi inafanyika  ikiwemo vyoo vya walimu pia, ambapo suala la  madawati  wanafunzi   robo tatu ya shule  hukalia magogo ya miti wakiwa darasani  yanahitajika madawati kwa wanafunzi hao.
Ofisa elimu msingi Andrew  Mitumba  wa halmashauri hiyo  alisema kuwa kero hiyo ni muda mrefu kwani mwalimu mkuu  alikwisha andikiwa barua ya  onyo kwa uzembe  kwa kutotekeleza changamoto  za ukosefu wa vyoo kwa wanafunzi haraka kwani  wazo la kuwa na shule linatoka kwenye serikali ya kijiji  na wizara inaridhia kwa kuangalia vigezo vyote kama vimetizmizwa ikiwemo vyoo, huu ni uzembe wa wananchi pamoja na  viongozi wa serikali ya kijiji.
“ Isitoshe  kuna  fedha za ruzuku hutolewa kwa shule za msingi ambazo anatakiwa  achukue kidogo na kuanzisha ujenzi ikiwemo na michango kwa wananchi  ili halmashauri iweze kukamilisha lakini  huyu mwalimu mkuu hafanyi hivyo kama alivyoelekezwa,pia suala la  ukosefu wa madawati  shuleni hapo lipo  kwani  halmashauri imetenga fedha kwaajili ya kupata madawati 513  na mipango ni kuzigawia shule ambazo  hazina  madawati sanjari na shule ya msingi hii  .
.

0 Response to "SHULE INAKABILIWA NA UKOSEFU WA CHOO CHA WANAFUNZI ZAIDI YA 500,PAMOJA NA WALIMU IKIWEMO MADAWATI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.