Habari za hivi Punde

WANANCHI WA VIJIJI VYA MWAKITOLYO NA MAWEMILU WALILIA MRADI WA MAJI WA ZIWA VICTORIA.

Maji haya ni mradi kutoka ziwa victoria ,pia wananchi wa vijiji vya Mwakitolyo na Mawemilu halmashauri ya (w)  Shinyanga walilia mradi kama huo.


WANANCHI wa vijiji vya Mwakitolyo  na Mawemilu  kata ya Mwakitolo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  wameanza kutekelezewa mradi wa  maji ya ziwa Victoria kutokana na  kukabiliwa na keroya uhaba wa maji  kwa muda mrefu hali ambayo inawafanya kupata maji ambayo siyo salama kutoka kwenye chemchem za kuchimba chini nayo hukauka  kwa muda mfupi.

Ahadi hiyo imeanza kutekelezwa kwa kusimamiwa na  mbunge wa jimbo hilo Amahed  Salum ikiwa tayari tenki la maji limeanza kukamilishwa lenye ujazo wa  lita 90,000  na kufaidisha wakazi zaidi ya 4000 ,uliogarimu jumla ya kiasi cha shilingi billion  1.36. ambapo maji hayo yatatengenezewa  mifereji ya kutoa maji ili kuweza kufikia  wakazi wa vijiji vyote  kwenye kata  hiyo.

Baadhi ya wananchi  wa vijiji  hivyo kwa nyakati tofauti  kilio hicho  kwenye mkutano wa hadhara kuhusu changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama  kwa mbunge  wao,ambapo  wakazi wa kijiji cha Mwakitolyo  walilalamika   kuchangishwa kiasi cha shilingi 39,000 kwa kila kaya ili kuweza kufanikisha mradi huo ikiwa walitaka ufafanuzi  kwanini wanachangishwa kiasi kikubwa  na kwa shughuli gani walihoji.

Mmoja wa wananchi hao  Vicenti Kusekwa alieleza mbele ya mbunge huyo kuwa  kero ya maji imekuwa ni tatizo kwa wananchi,pia mradi huo wameona kuanza kutekelezwa lakini umekuwepo uchangishwaji wa fedha kila kaya  ambazo hawafahamu zinatumika kufanya nini pia kiwango hicho kinachotamkwa ni kikubwa  hivyo walimtaka mbunge kuondoa kero hiyo ili waweze kupata maji.

Kwa upande wake mtendaji wa kata hiyo Goodluck Kipilimba  alitoa ufafanuzi kuwa  waliitisha mkutano wa hadhara  na kuwapatia maelezo yote kwa kina namna sheria inavyotakiwa jinsi ya kuchangia kwenye mradi ikiwa wananchi wanatakiwa kuchangia robo ya fedha zinazohitajika kwenye mradi huo ikiwa kijiji hiki kina kaya 942 na ukigawa kwa kiwango kinachotakiwa kila kaya itataikiwa kutoa shilingi 39,000.
Kaimu mhandisi wa maji Andrew  Mogella alielezwa kuwa mradi huo umegharimu jumla ya shilingi billion 1.3 na kunufaisha wakazi zaidi ya 4000  ikiwa ujanzo wa tanki hilo  ni lita 90,000 hivyo tayari ujenzi wa mifereji ya kupitisha mabomba imewekwa kwa lengo la kusambaza kwenye vijiji jirani na lililopo tanki hilo.

Mbunge huyo aliwataka kuunda kamati itakayosimamia fedha  za mradi wa maji yenye kuaminika kwani maeneo mengine  wamekuwa hawapeleki fedha benki wala kuwasomea mapato na matumizi ya fedha hizo  na matokeo yake huliwa hovyo, aliwaeleza  mradi huu uko mbioni kukamilika wasikubali kukaa miezi sita  bila kusomewa mapato hayo  ni ndani  ya mwezi mmoja  wasomewe ili kuweza kufamu kiasi cha pesa kinachopatikana.

“Mradi huo kuja niliupigia  kelele  kutoka wizarani,  ni mradi mkubwa kati ya miradi mitatu ndani ya jimbo la Solwa  ukianzia wa umeme  vijijini,ujenzi wa hospitali ya wilaya  na huu wa mwakitolyo  kila mmoja umegharimu kiasi cha fedha kisichopungua   billion  moja,hivyo mradi wa maji inatakiwa muwe makini nao na fedha zitakazo patika ni kwaajili ya matengenezo pindi pampu au pomba kukaribik”alisema mbunge Ahamed.

Alisema kuhusu uchangishwaji wa fedha hizo kiko sahihi kwani maeneo mengi yenye mradi yamechangishwa  ila kijiji hiki cha Mwakitolyo mnakiona kiwango hicho ni kikubwa kutokana na idadi ya kaya kuwa ndogo isitoshe haihusishi vijiji vingine ambvyo viko mbali na  tanki,ikiwa sheria iliyopo halmashauri katika mradi huu itachangia kiasi cha shilingi  million 36 na kingine wananchi wemyewe na asilimi 75 hutolewa na benki  ya dunia ambao ni wafadhili.
.

0 Response to "WANANCHI WA VIJIJI VYA MWAKITOLYO NA MAWEMILU WALILIA MRADI WA MAJI WA ZIWA VICTORIA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.