Habari za hivi Punde

HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA MKOANI TANGA IMEREJESHA WANAFUNZI 123 MASOMONI

NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI    PHILIPO  MULUGO.

HALMASHAURI ya Muheza mkoani Tanga ina mpango madhubuti wa kuwachukulia hatua kali za kisheria baadhi ya watu wanaowatumikisha wanafunzi kazi mbalimbali ikiwemo ya kuchuma machungwa na kupelekea kufanya utoro mashuleni.

Hatua hiyo imeibuka mara baada ya afisa elimu sekondari wa halmashauri ya wilaya ya Muheza,Lusajo Gwekisa alipokuwa akiwasilisha taarifa kwenye kikao cha baraza la madiwani iliyosema hatua zimeanza kuchukuliwa kwa wale wote ambao wamesababisha tatizo la utoro wa wanafunzi ambapo kesi 66 zimefunguliwa mahakamani huku wanafunzi 123 kati ya 303 wakirejeshwa masomoni.


Taarifa hiyo pia ilieleza kwamba hali hiyo ni sehemu ya mkakati wa utekelezaji wa agizo la Rais Jakata Kikwete ambapo ilisema kwamba kwa upande wa shule za msingi mpaka julai 27 mwaka huu wanafunzi wapatao 170 bado walikuwa hawajaweza kurejea masomoni huku juhudi zikiendelea.

Aidha taarifa hiyo iliendelea kueleza kwamba mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Muheza,Ibrahimu Matovu kwamba tayari ameshamwandikia barua hakimu mkazi mfawidhi kuhamishia mahakama kwenye maeneo ambayo hayana mahakama za mwanzo ili kuweza kushughulikia masuala ya mdondoko.

Wakati huo huo taarifa kutoka kwenye kikao hicho cha madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Muheza zinaeleza msako wa kuwanasa wale wanaowatumikisha watoto kwenye ajira zisizo rasmi unaendelea ambapo utekelezaji ulianza tangu tarehe 8 januari mwaka huu ambapo sheria itachukua mkondo wake.

Hata hivyo serikali imewataka wajumbe wa baraza la madiwani hapo katika maeneo yao kuhakikisha wana wabaini wazazi,walezi na baadhi ya wafanyabiashara wanawatumikisha wanafunzi na kuwalipa ujira na kusababisha wimbi kubwa la idadi ya utoro ambapo ni njia inayochangia kuwasababishia kutohudhuria masomo.

Baada ya kusomwa kwa taarifa hiyo ndipo ilimpelekea mkuu wa wilaya hiyo,Subira Mgalu kutoa rai hiyo kwenye kikao cha baraza la madiwani  kilichofanyika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Muheza huku akisema ushirikiano unahitajika kutoka kwa madiwani katika kuwafichua wamiliki wa mashamba ya machungwa sambamba na madalali ambao wamekuwa wakiwatumia wanafunzi kwa kazi hiyo.

Alisema kwamba katika wilaya ya Muheza kumezuka tatizo kubwa la ajira za utotoni suala ambalo limeonekana kuwa kikwazo kwa maendeleo  ya elimu ambapo vijana wengi wamekuwa wakikataa kuhudhuria shuleni kutokana na kwenda kweye mashamba kutumikishwa wakilipwa ujira mdogo na kuharibu maisha yao.

Mgalu alisema ili kuweza kukomesha vitendo hivyo vinavyozorotesha maendeleo ya sekta ya elimu madiwani wanatakiwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuvipatia taarifa zitakazowezesha watu wote wanaowatumikisha wanafunzi kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Akizungumzia zaidi tatizo la mdondoko wa wanafunzi,Mgalu alisema ili kuliondosha viongozi wanapaswa kulifanya kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao vyao licha ya kuwepo kwa mafanikio ya kuanza  kurejeshwa madarasani kwa baadhi ya wanafunzi waliotoroka shule huku akisisitiza zoezi kuwa ndelevu.

0 Response to "HALMASHAURI YA WILAYA YA MUHEZA MKOANI TANGA IMEREJESHA WANAFUNZI 123 MASOMONI "

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.