Habari za hivi Punde

KANISA LA KKKT KUNYANYUA VIJANA KATIKA TATIZO LA AJIRA.

KANISA la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Jimbo la Kusini Magharibi limeadhimia kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana wanaokomea kidato cha nne kwa kujenga Shule ya Sekondari ya Ufundi itakayotoa mafunzo ya stadi za maisha.

Hayo  yalielezwa na Mkuu wa Jimbo la Kusini Magharibi;Mchungaji Daniel Mono katika taarifa aliyoisoma mbele ya Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria,Askofu Emmanuel Makala,wakati wa kuweka Wakfu ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Agape Lutheran.


Mchungaji Mono alisema ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Agape utakayojengwa kwa awamu nne utagharimu jumla ya Shilingi 520,623,740/= ambapo shule hiyo itakuwa msaada mkubwa wa kumudu kujitegemea kimaisha kwa vijana watakaobahatika kusomea shule hiyo.

Alisema lengo kubwa la kuanzishwa kwa sekondari hiyo ni kuwapatia wanafunzi masomo ya ziada ya ufundi ambayo ana hakika yatakuwa mkombozi mkubwa wa kuondokana na maisha ya utegemezi kama walionayo vijana wengi waliokomea kidato cha nne.

Aidha alisema sekondari hiyo ambayo ni zao la Agape Lutheran Primary School,kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo imemudu kufaulisha kwa darasa zima kwa vijana waliomaliza elimu ya msingi hupoteza mwelekeo wao wa kitaaluma kutokana na kukabiliana na mazingira mapya yanayowabadirisha kimaadili kutoka waliyozoea ya Kanisa.

Mchungaji huyo alisema matarajio ya Sekondari hiyo ni kuanza January 2016,ambapo mbali na kuwajengea vijana stadi za maisha ili kuondokana na dhana ya kuajiriwa pia itakuwa msaada mkubwa kwa maendeleo ya Dayosisi kwa kuongeza  uthamani  na majengo pindi wanapokuwa katika mafunzo ya vitendo.

Akifafanua hatua za ukamilishaji wa Sekondari hiyo,awamu itahusu madarasa manne na ofisi ambayo itakayo gharimu  zaidi ya shilingi millioni mia moja,awamu ya pili itahusu ujenzi wa jiko  na kugharimu Shilingi  millioni 150

Awamu ya tatu itakuwa ni kujenga jengo la Utawala na Karakana ya ufundi itakayogharimu pia Shilingi  millioni 150 huku awamu ya mwisho itakayohusu nyumba za walimu ambazo zitagharimu Shilingi millioni 120, hivyo kuwaomba wafadhili na marafiki wa kanisa kujitokeza kuchangia ili kukamilisha kwa wakati sekondari hiyo.

Nae Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania “KKKT”Jimbo la Kusini Magharibi;Emmanuel Makala aliwaasa watakaosimamia ujenzi huo kuwa waadirifu na kuhakikisha mradi huo unakuwa na akaunti yake isiyoingiliana na ya miradi mingine ya Kanisa.

Askofu Makala katika kuhakikisha hilo linafanyika alianzisha Harambee ya ufunguzi wa akaunti hiyo ambapo zilipatikana kiasi cha Shilingi Milioni Moja taslimu.


0 Response to "KANISA LA KKKT KUNYANYUA VIJANA KATIKA TATIZO LA AJIRA."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.