Habari za hivi Punde

MABWENI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA MIMBA UTORO MASHULENI KWA WANAFUNZI WA KIKE.

HILI NI  JENGO LA BWENI LA WASICHANA  KATIKA SHULE YA SKONDARI USULE HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA.
SHULE ya sekondari  Usule iliyopo katika kijiji cha  Masekelo kata ya  Bukene   halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  imeanza ujenzi wa bweni la wasichana lengo ni kupunguza utoro na mimba  kwa wanafunzi  wa kike ambalo ndilo limekuwa changamoto kubwa  shuleni hapo.

Ujenzi huo ambao ndio umeanza na kufikia hatua ya lenta  umegaharimu  kiasi cha shilingi  millioni 36 ambazo zimetolewa na halmashauri  ikiwa zinahitajika kiasi cha shilingi millioni 12 ili kuweza kukamilisha ujenzi huo  ambapo bweni hilo linatarajia kuchukua wanafunzi zaidi ya 40 pindi litakapokamilika.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo  Paulo Maganya  alisema kuwa  ujenzi wa hostel utachangia kupunguza utoro na mimba shuleni hapo kwa wanafunzi wa kike ikiwa kwa mwaka huu wanafunzi watano walibainika kuwa na mimba,huku suala la utoro likikuwa kwa kasi  kubwa kutokana na umbali mrefu kwa wanafunzi kutembea  ingawa hutumia usafiri  wa  baiskeli   wakati mwingine huchoka na kujikuta hawahudhurii shuleni.
“Shule hii inawanafunzi  350 ikiwa wasichana ni 200 na wavulana 150, matokeo ya kidato cha  nne kwa mwaka huu  yalikuwa mazuri  waliofaulu wasichana ni 11 na wavulana 8 na kuifanya shule hiyo kuwa  ya tatu kiwilaya ,hivyo  kama bweni la wasichana likikamilika  litaweza kudhibiti utoro na mimba kwani wanafunzi hao wamekuwa wakitembea umbali mrefu  inayowafanya kuchoka hiyo ndiyo tumeona ni sababu mojawapo”alisema  Maganya.
Naye kaimu ofisa mtendaji wa kata hiyo Edward Ndono baada ya kuwasili mbunge wa jimbo la Solwa Ahamed Salum  na  kuweka jiwe la msingi katika  bweni hilo alisoma taarifa juu ya shule hiyo ambapo alieleza changamoto zinazowakabili kuwa ni  uhaba wa maji, mimba kwa wanafunzi  ikiwemo fedha za kukamilisha bweni hilo sanjari na jengo la utawala lililoanza ujenzi wake tangu mwaka 2006.
Pia ofisa elimu  sekondari  kutoka  halmashauri hiyo  Karugoba  Jesse  alisema kuwa  suala la mimba mashuleni limekuwa ni changamoto kubwa  ujenzi wa mabweni utaweza kusaidia kupunguza tatizo hilo kwa kushirikiana na wazazi katika dhana nzima ya  maadili, na kila baada ya miezi mitatu  idadi ya wanafunzi watano mpaka saba kwa  halmashauri nzima  wanapatikana na mimba  wakiwa shuleni.
Mbunge huyo kwanza aliwataka wazazi na walezi kuwapa maadili watoto wao na kuwaeleza madhara ya mimba za utotoni kwani wamekuwa hawatumii hata kinga matokeo yake kupata mimba jambo ambalo ni hatari,pia  suala la kukamilisha hosteli atatoa kiasi cha shilingi millioni sita na halmashauri millioni sita ili kuweza  kupatikana kiwango kinachotakiwa na ujenzi kukamilika.
“Mimi nitatoa kiasi cha shilingi millioni sita na halmashauri kiasi cha shilingi millioni sita  ili kuweza kukamilisha ujenzi huo, tatizo la mimba kwa wanafunzi ni kubwa hivyo wazazi na walezi  mnatakiwa kutoa elimu ya maadili kwa watoto ili kutoweza kubeba mimba wakiwa shuleni  kwa kushirikina hilo linawezekana”alisema Mbunge Salum.


0 Response to "MABWENI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA MIMBA UTORO MASHULENI KWA WANAFUNZI WA KIKE."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.