Habari za hivi Punde

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA TANGA KUPANDISHA TOZO LA MAJI.

MAMLAKA ya maji safi na utunzaji wa mazingira Tanga Uwasa mkoani Tanga ina mpango wa kupandisha tozo za maji na kufanyia ukarabati wa miundombini ili kuondoa uchakavu uliopo uliojengwa tangu ukoloni.

Mkurungezi Mtendaji wa Mamlaka hiyo ya maji safi na utunzaji wa mazingira wa Tanga Uwasa,Injinia,Joshua Mgeyekwa akizungumza juzi katika kikao cha wadau kilichofanyika ukumbi wa CCM mkoani hapo alisema lengo ni kuboresha na kuwaondolea adha inayojitokeza kwa watumiaji wao hasa kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la kange.


Pia alitumia nafasi hiyo  kuwatoa shaka wadau wa maji kwamba ni mpango huo wa kuongeza bei ya huduma za maji kwa vipindi vya miaka mitatu mfululizo unalengo la kuongeza huduma na kasi ya upatikani wa maji kwenye maeneo mengi hasa yaliyopanuka zaidi.

Mgeyekwa alibainisha kwamba kutokana na kuwa na ongezeko kubwa la watu na hawana nia mbaya ya kumkomoa mkazi wa Tanga bali ni kumuhakikishia huduma hiyo ya upatikanji wa maji inapatikana kama ilivyokusudiwa kwa watumiaji.

Alisema kwamba ili kukabiliana na kuondoa tatizo hilo kwa wadau wao mamlaka imepelekea kuomba kupandisha tozo hizo za maji sambamba na ukarabati njia pekee itakayoweza kutoa huduma hiyo kwa tija.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Halima Dendego alisema mpaka ifikapo June mwaka 2015  itakuwa imejihakikishia kusambaza  huduma ya majisafi na salama  kwenye maeneo yote yaliyoko mjini na vijijini  kwa zaidi ya asilimia 99.

Alisema kuwa mpaka sasa miradi ya usambabazaji maji ya vijiji kumi iliyotoka na fedha kutoka Benki ya dunia ipo katika hatua za mwisho za kukamilika hali inayotuma uhakika wa huduma hii kuwa itapatika kwa kiwango kikubwa.

Dendego pia alibainisha kwamba kwa kiasi kikubwa wilaya ya Tanga haitakuwa na shida ya maji kutoka na mipango iliyopo ya kuendelea kusogeza huduma hii karibu ikiwemo maeneo ya mjini kulikuwa hakuna shida ila tabu lilikuwepo vijijini lakini nako litakuwa historia.

Hata hivyo baadhi ya wadau waliohudhulia waliopata fursa ya kuhudhulia mkutano huo waliipongeza Tanga Uwasa kwa hatua hiyo na kuitaka kuhakikisha huduma hiyo inakwenda sambamba na tozo watakayoitoa badala ya kuwa tofauti na walichoahidi kwao.

0 Response to "MAMLAKA YA MAJI SAFI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA TANGA KUPANDISHA TOZO LA MAJI."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.