Habari za hivi Punde

MBUNGE JOHN SHIBUDA ATOA YA MOYONI MWAKE,ATANGAZA VITA DHIDI YA TUNDU LISSU.


Siku chache baada ya Mbunge wa Maswa Magharibi John Shibuda (CHADEMA) kudaiwa kuusaliti Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwa kurudi katika bunge la katiba linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma, na kuwepo taarifa za kufukuzwa ndani ya Chama chake (CHADEMA) Mbunge huyo imeibuka na kusema kuwa amechoswa na Chama hicho.


Chibuda amesema kuwa amechoka kutukanwa, kuitwa msaliti, mnafiki huku akibainisha kuwa kamwe hawezi kuvumilia vitendo hivyo na kubainisha kuwa matusi ambayo yametolewa juu yake sasa yametosha.


Mbunge huyo aliyasema hayo jana wakati akiongea na waandishi wa habari pamoja na Baraza la wazee Wilayani Maswa Mkoani Simiyu, na kutangaza rasmi kuachana na chama hicho.


Alisema tangu amejiunga na chadema amekuwa mtu wa kutukanwa na kuitwa masaliti kila mara, ikiwa pamoja na kunyimwa ushirikiano kutoka katika uongozi wa juu wa chama hicho katika kukiletea maendelea na wananchi kwa ujumla.


Alibainisha kuwa chadema kimeshindwa kumpa heshima aliyona nayo, hivyo kubainisha kuwa hawezi kuendeshwa kama mtoto na wala kupelekwa kama viongozi wa chama hicho wanavyotaka.


“tangu nimejiunga chama hiki..kila siku ni matusi kwangu..hata watoto wadogo ndani ya chama hiki nao wamediriki kunitukana..sasa nimechoka na siwezi kuvumilia hali hii..nimekuwa mvumilivu kwa muda mrefu..natanga kuwa sitagombea ubunge nikiwa Chadema na cha hiki siyo baba wala mama yangu” Alisema Shibuda.


Kuhusu kurudi Bungeni.
Akiongelea juu ya taarifa za kurudi bungeni mwanasiasa huyo alisema kuwa taarifa hizo siyo za kweli na hajawahi kuingia ndani ya bunge hilo, bali alipita wakati akitokea Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa matibabu.


Alibainisha kuwa wakati akitokea mkoani Dar es Salaam afya yake ilikuwa mbaya, ikiwemo kuvimba miguu, hali iliyomlazimu kupia kupita kwa madaktari walioko ndani ya viwanja vya bunge ili kupewa dawa na kuangaliwa afya yake.


“wakati nipo njiani nakuja Maswa kwenye Msiba afya yangu ilikuwa mbaya..nikaamua kumpigia simu daktari pale bungeni juu ya afya yangu..akaniambia nipite akanicheki..nilipofika bungeni nikapewa maelekezo ili niweze kupata dawa na kuangaliwa afya yangu ni lazima nijiandikishe” alisema na kuongeza kuwa..


“nami sikukataa kujiandakisha nilipomaliza utaratibu wa kujiandikisha nilipewa dawa na kuangaliwa afya yangu..na watu waliponiona hapo bungeni wakasema nimewasaliti UKAWA jambo ambalo siyo kweli”


Alisema alipomaliza kupata dawa aliendelea na safari yake kuja katika jimbo lake kwa ajili ya msiba, ambapo alieleza kushangaa kusikia kuwa karudi bungeni wakati yuko msibani.


Kuhusu UKAWA.
Akiongelea juu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) waliogoma kurudi bungeni, Shibuda alisema kuwa umoja huo hauna maslai kwa watanzania ambao alisema asilimia kubwa ni wakulima na wafugaji.


Alibainisha kuwa tangu watoke ndani ya bunge hilo na yeye akiwa mmoja ya waliotoka, hajawahi kujulishwa jambo lolote juu ya mwenendo wa mazungumzo baina ya umoja huo na CCM.


Alisema kitendo cha kutojurishwa jambo lolote kimekuwa kikimpa shida ya kuamua kuendelea na bunge au kususia, kutokana na kutopewa taarifa za mchakato wa maridhiano, huku akibainisha kuwa wajumbe wengine wamekuwa wakipata taarifa hizo na yeye kubaguliwa.


“mimi siyo mkokoteni..na siwezi nikaota juu ya maamuzi ya UKAWA ambayo wamekuwa wakiyajadili katika vikao vya maridhiano..wajumbe wengine wamekuwa wakipewa taarifa kila siku na kinachoendelea mpaka sasa…lakini mimi nabaguliwa kwa nini?” Alisema


Aidha aliuponda umoja huo kwa kusema kuwa hauna maslai kwa wakulima wa pamba, pamoja na wafugaji, ambao alisema ndiyo wapiga kura wake na ambao walimtuma bungeni kujadili kero zao.


Atangaza kurudi bungeni.
Katika hali isiyo ya kawaida Mbunge huyo alitangaza rasmi kuendelea na vikao vya bunge maalumu la katiba, kwa madai kuwa anaenda kuzungumzia kero za wakulima wa pamba pamoja na wafugaji ili ziwekwe katika katiba mpya.


“mimi nipelekwi pelekwi…na wala siko tayari kupelekwa na chama chochote hapa nchini wala viongozi..nasema nitaenda bungeni wiki hii..kuendelea na vikao niwatetee wakulima wangu wa pamba pamoja na wafugaji ambao ni maskini sana” Alisema.


Juu ya viongozi wa Chadema.
Akiongelea juu ya uongozi ndani ya chama hicho alisema kuwa viongozi wamekuwa wakitumia ubabe, vitisho, pamoja na ubaguzi katika kukiendesha chama, huku akieleza kuwa viongozi hao wamekuwa hawana hekima na busara.


Alibanisha viongozi hao wamekuwa wakitumia ubabe na kuwaendesha wanachama wao pamoja na wabunge wao kama watumwa na kuwataka kufanya watakavyo kwa maslai ya kwao binafsi.


“chadema viongozi wote ni wababe, hawana hekima na busara wanataka kuendesha chama watakavyo, kama cha kwao...mimi hiyo nimekataa. nataka niwaambie viongozi hao waliposikia nimetoka CCM wao ndiyo walinifuata nijiunge na chama chao” Alisema


Atangaza vita dhidi ya Tundu Lissu.
Akiongea kwa asira kali, mbunge huyo alibainisha kukerwa na mwanasheria wa chama hicho na mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, kwa kuendelea kumwandama bila ya sababu maalumu na kumtaka kuacha mara moja vitendo hivyo.


Alisema amemvumilia kwa kiwango kikubwa mbunge huyo, ambapo alitangaza kuanzisha vita dhidi yake juu ya kinachoendelea katika kumuongelea uongo mbao hauna faida yeyote.


“Lissu amenishtumu mengi nimemsikiliza sana..na nimemvumilia vya kutosha..sasa ndani ya siku chache nikirudi Dar es Salaam tutaonana..maana mimi siwezi kutukanwa na mtoto mdogo kama Lissu” Alisema.


Shibuda mbali na kutangaza kukiama chama hicho hakuwa tiyari kuzumgumzia chama atakachoamia, ambapo alibainisha kuwa chama atakachoamia bado ni siri yake, huku akibainisha kuwa kitakuwa chama kipya hapa nchini.


Wazee wamuunga mkono.
Nao wazee waliohudhulia Mkutano huo walimuunga mkono mbunge huyo kwa uhamuzi wake wa kikiama chama hicho, huku wakimtaka kurejea bungeni kwa ajili ya kutetema wananchi wa maswa ambao ni wakulima na wafugaji.


“sisi kama wazee tunakuunga mkono mbunge wetu..na tunawataka wabunge wengine kurejea bungeni kujadili matatizo ya watanzania..watanzania matatizo yao siyo muundo wa serikali..tunataka wakulima na wafugaji wadhaminiwe” Alisema Mohamed Mangasiri Mwenyekiti Baraza la wazee Maswa.


0 Response to "MBUNGE JOHN SHIBUDA ATOA YA MOYONI MWAKE,ATANGAZA VITA DHIDI YA TUNDU LISSU."

Post a Comment

KARENY. Powered by Blogger.